Makamu mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania bara Philip Mangula (72), hatimaye amefunga ndoa na mkuu wa shule ya sekondari ya Philip Mangula iliyopo kata ya Imalinyi wilayani Wanging’ombe mkoani hapa, Yolanda Kabelege (54).
Ndoa ya Mzee Mangula na Mwalimu Yolanda imefungwa jana majira saa 8 mchana katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT) mjini Njombe, ambapo misa ya ibada ya ndoa hiyo iliongozwa na Askofu Mstaafu wa KKKT dayosisi ya kusini Njombe Solomon Swalo pamoja na Askofu Isaya Mengele wa diyosisi hiyo.
Source: Matukio Daima
No comments:
Post a Comment