Pages

Friday, January 4, 2013

Papi Kocha amuangukia JK


 
MF/NA: 836'04|Johnson Nguza (Papii Kocha)
Gereza Kuu Ukonga
S.L.P 9091
Dar es Salaam
                         
                                Mh. Rais wa Jamuhuri ya MuunganoTanzania
 
YAH: MAOMBI YA KUPEWA MSAADA (MSAMAHA) WA KUFUTIWA ADHABU YA KIFUNGO NILIYOPEWA NA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU.

Husika na somo hilo hapo juu. Mimi ni mfungwa katika gereza kuu la Ukonga. Kwa heshima na taadhima na kwa kutambua utu na huruma yako ya ki MUNGU ulionayo dhidi ya binadamu wenzako pamoja na mamlaka uliyokabidhiwa na jamuhuri ya muungano wa Tanzania, naanguka na kushika miguu yako mitukufu muheshimiwa rais.

Na kuomba msaada (msamaha) kwako muheshimiwa rais Kwa njia hii ya maandishi kusudi niweze kuondolewa adhabu ya kifungo cha maisha gerezani, niliyohukumiwa na mahakama tajwa hapo juu. Mh.Rais mimi nimefungwa nikiwa bado kijana mwenye umri mdogo, mpaka sasa natambua wazi hatima pamoja na dhamana ya maisha yangu ipo katika mikono yako mitukufu Mh. Rais.

Naomba huruma yako muheshimiwa Rais maana mimi ni mtoto wako ninaehitaji huruma yako wewe mzazi. Natumaini kauli yako ya mwisho ndio itakayoleta pumzi ya uhai nafsini mwangu Nakutakia kazi njema, afya njema na maisha marefu.

Mungu akubariki Wako mtiifu
NO:836'04 JOHNSON NGUZA
(PAPII KOCHA)

Angalia barua iliyoandikwa kwa mkono hapa: http://ladyjaydee.blogspot.com/2010/02/nimetumiwa-barua-na-papii-kocha-toka.html

1 comment: