
- Akiri kushiriki pamoja na akina Lukuvi
- Akwepa kuzungumzia meseji za matusi
MNADHIMU Mkuu wa Kambi ya Upinzani Tundu Lissu amefichua mwenendo wa mjadala wa kikao kilichofikia uamuzi wa kufuta Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) iliyokuwa ikiongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA).
Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA) amezungumza na Raia Mwema kujibu madai kwamba yeye aliunga mkono hoja ya kufutwa kwa kamati hiyo wakati wa kikao cha Kamati ya Kanuni za Bunge na alifanya hivyo kusimamia msimamo wa chama chake, unaodaiwa kuungwa mkono na baadhi ya viongozi wa juu, ikiaminika ilikuwa njia ya kuzidi kumdhibiti Zitto kisiasa.
Lakini ameyapingwa madai hayo akieleza mwenendo wa mjadala kuhusu hoja hiyo na kiwango cha upinzani alioonyesha.
Mbali na Lissu, kamati ambayo ilipitisha uamuzi huo inaundwa na Mbunge wa Mbulu (CHADEMA) Mustafa Akuunay; Mbunge wa Kibondo, Felix Mkosamali (NCCR-Mageuzi); Mbunge wa Mkanyageni, Habib Mnyaa (CUF); Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohammed (CUF); Mbunge wa Tunduru Kaskazini, Mhandisi Ramo Makani (CCM); Mbunge wa Viti Maalumu, Pindi Chana (CCM) na Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM). Vikao vya kamati hiyo vinaongozwa na Spika.
Maelezo ya Lissu
Mazungumzo kati ya Lissu na mwandishi wetu baada ya utambulisho na maelezo ya awali yalikuwa hivi;
Mwandishi: Ulishiriki katika kikao cha Kamati ya Kanuni za Bunge na unadaiwa kuunga mkono hoja ya kuvunjwa kwa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma. Ni kweli?
Lissu: Kweli nilishiriki, lakini sikuunga mkono hiyo hoja. Nilisema sababu za kuanzishwa kwa kamati hiyo bado hazijapitwa na wakati, tena zina uzito mkubwa zaidi kwa sasa.
Kisheria Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) anatoa ripoti za ukaguzi tatu. Kwanza Kamati ya Hesabu za Serikali Kuu, pili; Hesabu za Mashirika ya Umma na tatu; Hesabu za Serikali za Mitaa. Si sahihi kuua kamati moja na kuacha nyingine mbili.
Mwandishi: Kama si sahihi ulikuwa na mapendekezo gani mbadala?
Lissu: Nilisema ni bora ziunganishwe kamati zote tatu au kuacha kama ilivyokuwa. Mapendelezo yalikataliwa...kama unavyojua wao wapo wengi kwa idadi kwa hiyo walipitisha uamuzi.
Mwandishi: Lakini wanasema lengo la kuunganisha kamati ni kutoa fursa kwa wizara na mashirika inayosimamia kuripoti sehemu moja. Kwa mfano, kabla ya kuvunja Waziri wa Nishati aliwajibika Kamati ya Hesabu Serikali Kuu na TANESCO, shirika lililo chini yake liliwajibika Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma. Huoni kuna mantiki?
Lissu: Hiyo hoja haikuletwa kwenye Kamati ya Kanuni za Bunge, imejitokeza huku mtaani. Lakini hata hivyo, haina nguvu kwa sababu kuna wizara nyingi ambazo zinawajibika katika kamati zaidi ya moja bungeni.
Mwandishi: Uamuzi gani zaidi wa kibunge mtakaochukua?
Lissu: Hakuna uamuzi zaidi kwa sababu rufaa zote za kibunge zinakatwa kwenye Kamati ya Kanuni za Bunge na chombo hicho ndicho kimeamua kuvunja kamati hizo, hapa ni kuzidi kuchukua uamuzi wa kisiasa.
Meseji matusi kwa Spika
Kuhusu ujumbe mfupi wa simu ya mkononi uliotumwa kwa Spika Anna Makinda unaodaiwa kuwa wa matusi ya nguoni, kama ilivyopotiwa na baadhi ya magazeti jana Jumanne, Lissu alisema hawezi kutoa maoni yoyote kuhusu suala hilo.
“Bado sijaonyeshwa hizo meseji zinazoitwa za matusi. Ningeonyeshwa ningeweza kutoa maoni yangu kwa sababu wewe unaweza kudhani ni matusi kumbe si matusi. Kwa hiyo sina maoni hadi nitakapoonyeshwa,” alisema Lissu ambaye akiwa bungeni, Spika wa Bunge, Makinda alimtaja kama ndiye kinara wa vurugu ndani ya ukumbi wa Bunge.
Moto wazidi kusambaa
Uamuzi huo wa Spika kupitia Kamati ya Kanuni za Bunge ambao Lissu anasema ni ushahidi mwingine wa matumizi mabaya ya kanuni za Bunge, umezidi kuwa mwiba kwa uongozi wa Bunge licha ya kwamba ni uamuzi uliopitia hatua zote za kibunge.
Inaelezwa kwamba baadhi ya mabalozi nchini wameanza kufuatilia sababu hasa za kufikiwa kwa uamuzi huo, ikizingatiwa ya kwamba lengo la kamati hiyo pamoja na nyingine ni kudhibiti matumizi ambayo yanatokana na Bajeti inayochangiwa na baadhi ya nchi wahisani.
Taarifa zinaeleza kuwa, Zitto Kabwe anaweza kupata fursa ya kujieleza mbele ya wahisani nchini na anaweza kufanya hivyo katika kikao kilichoandaliwa Alhamisi, wiki hii jijini Dar e Salaam.
Akizungumzia uamuzi huo, mmoja wa wadau alisema; “Mapendekezo ya CAG katika taarifa ya mashirika ya umma ya mwaka 2011 yanasema Bunge linapaswa kupanua majukumu Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Uma katika kuhakikisha kamati inakuwa na nguvu ya kikanuni za Bunge katika kusimamia hesabu za mashirika na kampuni zote ambazo serikali ina hisa. Hata kama serikali inamiliki asilimia chini ya 50.”
Lakini mmoja wa wabunge ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini alisema; “Sijui kwa nini watu wanahangaika, Bunge kupitia Kamati ya Kanuni haikufuta shughuli za iliyokuwa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma bali kilichofanyika ni kuhamishia majukumu hayo katika kamati nyingine ili kupata ufanisi zaidi.”
Mbali na Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma kuunganishwa na Kamati ya Hesabu za Serikali Kuu, Kamati nyingine iliyoundwa ni iliyokuwa Kamati ya Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje ambayo imemegwa na kuundwa kamati mbili, moja ni Ulinzi na Usalama na nyingine ni Kamati ya Mambo ya Nje.
Source:Raia Mwema
Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA) amezungumza na Raia Mwema kujibu madai kwamba yeye aliunga mkono hoja ya kufutwa kwa kamati hiyo wakati wa kikao cha Kamati ya Kanuni za Bunge na alifanya hivyo kusimamia msimamo wa chama chake, unaodaiwa kuungwa mkono na baadhi ya viongozi wa juu, ikiaminika ilikuwa njia ya kuzidi kumdhibiti Zitto kisiasa.
Lakini ameyapingwa madai hayo akieleza mwenendo wa mjadala kuhusu hoja hiyo na kiwango cha upinzani alioonyesha.
Mbali na Lissu, kamati ambayo ilipitisha uamuzi huo inaundwa na Mbunge wa Mbulu (CHADEMA) Mustafa Akuunay; Mbunge wa Kibondo, Felix Mkosamali (NCCR-Mageuzi); Mbunge wa Mkanyageni, Habib Mnyaa (CUF); Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohammed (CUF); Mbunge wa Tunduru Kaskazini, Mhandisi Ramo Makani (CCM); Mbunge wa Viti Maalumu, Pindi Chana (CCM) na Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM). Vikao vya kamati hiyo vinaongozwa na Spika.
Maelezo ya Lissu
Mazungumzo kati ya Lissu na mwandishi wetu baada ya utambulisho na maelezo ya awali yalikuwa hivi;
Mwandishi: Ulishiriki katika kikao cha Kamati ya Kanuni za Bunge na unadaiwa kuunga mkono hoja ya kuvunjwa kwa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma. Ni kweli?
Lissu: Kweli nilishiriki, lakini sikuunga mkono hiyo hoja. Nilisema sababu za kuanzishwa kwa kamati hiyo bado hazijapitwa na wakati, tena zina uzito mkubwa zaidi kwa sasa.
Kisheria Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) anatoa ripoti za ukaguzi tatu. Kwanza Kamati ya Hesabu za Serikali Kuu, pili; Hesabu za Mashirika ya Umma na tatu; Hesabu za Serikali za Mitaa. Si sahihi kuua kamati moja na kuacha nyingine mbili.
Mwandishi: Kama si sahihi ulikuwa na mapendekezo gani mbadala?
Lissu: Nilisema ni bora ziunganishwe kamati zote tatu au kuacha kama ilivyokuwa. Mapendelezo yalikataliwa...kama unavyojua wao wapo wengi kwa idadi kwa hiyo walipitisha uamuzi.
Mwandishi: Lakini wanasema lengo la kuunganisha kamati ni kutoa fursa kwa wizara na mashirika inayosimamia kuripoti sehemu moja. Kwa mfano, kabla ya kuvunja Waziri wa Nishati aliwajibika Kamati ya Hesabu Serikali Kuu na TANESCO, shirika lililo chini yake liliwajibika Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma. Huoni kuna mantiki?
Lissu: Hiyo hoja haikuletwa kwenye Kamati ya Kanuni za Bunge, imejitokeza huku mtaani. Lakini hata hivyo, haina nguvu kwa sababu kuna wizara nyingi ambazo zinawajibika katika kamati zaidi ya moja bungeni.
Mwandishi: Uamuzi gani zaidi wa kibunge mtakaochukua?
Lissu: Hakuna uamuzi zaidi kwa sababu rufaa zote za kibunge zinakatwa kwenye Kamati ya Kanuni za Bunge na chombo hicho ndicho kimeamua kuvunja kamati hizo, hapa ni kuzidi kuchukua uamuzi wa kisiasa.
Meseji matusi kwa Spika
Kuhusu ujumbe mfupi wa simu ya mkononi uliotumwa kwa Spika Anna Makinda unaodaiwa kuwa wa matusi ya nguoni, kama ilivyopotiwa na baadhi ya magazeti jana Jumanne, Lissu alisema hawezi kutoa maoni yoyote kuhusu suala hilo.
“Bado sijaonyeshwa hizo meseji zinazoitwa za matusi. Ningeonyeshwa ningeweza kutoa maoni yangu kwa sababu wewe unaweza kudhani ni matusi kumbe si matusi. Kwa hiyo sina maoni hadi nitakapoonyeshwa,” alisema Lissu ambaye akiwa bungeni, Spika wa Bunge, Makinda alimtaja kama ndiye kinara wa vurugu ndani ya ukumbi wa Bunge.
Moto wazidi kusambaa
Uamuzi huo wa Spika kupitia Kamati ya Kanuni za Bunge ambao Lissu anasema ni ushahidi mwingine wa matumizi mabaya ya kanuni za Bunge, umezidi kuwa mwiba kwa uongozi wa Bunge licha ya kwamba ni uamuzi uliopitia hatua zote za kibunge.
Inaelezwa kwamba baadhi ya mabalozi nchini wameanza kufuatilia sababu hasa za kufikiwa kwa uamuzi huo, ikizingatiwa ya kwamba lengo la kamati hiyo pamoja na nyingine ni kudhibiti matumizi ambayo yanatokana na Bajeti inayochangiwa na baadhi ya nchi wahisani.
Taarifa zinaeleza kuwa, Zitto Kabwe anaweza kupata fursa ya kujieleza mbele ya wahisani nchini na anaweza kufanya hivyo katika kikao kilichoandaliwa Alhamisi, wiki hii jijini Dar e Salaam.
Akizungumzia uamuzi huo, mmoja wa wadau alisema; “Mapendekezo ya CAG katika taarifa ya mashirika ya umma ya mwaka 2011 yanasema Bunge linapaswa kupanua majukumu Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Uma katika kuhakikisha kamati inakuwa na nguvu ya kikanuni za Bunge katika kusimamia hesabu za mashirika na kampuni zote ambazo serikali ina hisa. Hata kama serikali inamiliki asilimia chini ya 50.”
Lakini mmoja wa wabunge ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini alisema; “Sijui kwa nini watu wanahangaika, Bunge kupitia Kamati ya Kanuni haikufuta shughuli za iliyokuwa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma bali kilichofanyika ni kuhamishia majukumu hayo katika kamati nyingine ili kupata ufanisi zaidi.”
Mbali na Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma kuunganishwa na Kamati ya Hesabu za Serikali Kuu, Kamati nyingine iliyoundwa ni iliyokuwa Kamati ya Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje ambayo imemegwa na kuundwa kamati mbili, moja ni Ulinzi na Usalama na nyingine ni Kamati ya Mambo ya Nje.
Source:Raia Mwema
No comments:
Post a Comment