Mbunge wa Kigoma kaskazini na naibu katibu mkuu wa CHADEMA mh Zitto Kabwe jana alikituhumu wazi wazi Chama Cha Mapinduzi kuwa ndio kiini cha udini unaoanza kuligubika taifa la Tanzania lililokuwa linasifika kwa amani.
Akichangia hoja ya makadirio ya bajeti ya wizara ya mambo ya Ndani jana usiku Bungeni mjini Dodoma, Zitto alisema CCM imekuwa na tabia ya kuvihusisha vyama vya upinzani vyenye nguvu na udini. "Wakati chama cha wananchi CUF kilipokuwa na nguvu kilihusishwa na dini ya kiislamu, vivyo hivyo kwa CDM ambacho kinahusishwa na dini ya kikristo pamoja na ukanda" alisema Mh Zitto.
"Hali hii bila kujua ndi imeleta mifarakano ya kidini miongoni mwa jamii yetu hivyo kupelekea kuwa na chuki kubwa miongoni mwa dini hizi mbili na kusababisha matukio ya ajabu kutokea katika nchi yetu" Alisema Mh Zitto.
Hata hivyo Zitto kwa kiasi kikubwa aliwalaumu viongozi wote kwa ujumla kuacha kutoa hotuba zenye kuchochea chuki miongoni mwa jamii ya Tanzania na kubadilika mara moja ili kuijenga upya jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo kwa sasa ina nyufa nyingi zinazoweza kuliangusha taifa hilo nguli la Amani.
No comments:
Post a Comment