Pages

Friday, July 26, 2013

Mjasiriamali na Mfanyabiashara


Habari wana blog:

Chapisho la mwisho tuliona kwa ufupi na maana nyepesi ya neno ujasiriamali na kuangalia jinsi mjasiriamali anavyowezesha kutumia rasilimali ardhi, watu, maji na mtaji kuweza kufanya uzalishaji aidha wa mazao (bidhaa) ama kutoa huduma kwa lengo la kujipatia faida.
 
Ubunifu
Bado neno Mjasiriamali linaweza kuwa na maana nyingi ikiwemo ya uwezo wa mtu (mfanyabiashara) kubuni (innovations) kitu (vitu) vipya na kuvitambulisha katika jamii inayomzunguka katika jitihada ya kufanya vitu hivyo viwe na uwezo wa kujikwamua kiuchumi.
 
Kumbuka sio wafanyabiashara wote ni wajasiriamali, ila wajasiriamali wote ni wafanyabishara. Sifa mojawapo ya mjasiriamali ni kuwa mbunifu wa vitu vipya (bidhaa ama huduma). Huduma kama njia mojawapo ya kupata faida ni kama vile haifahamiki miongoni mwa watanzania wengi. Wengi wetu hufikiri ili uweze kupata kipato ni vyema ukauza bidhaa, huku utoaji wa huduma ukiachwa kwa watu wachache ambao hutumia fursa hiyo kupata faida kubwa.
 
Hivyo ubunifu huweza kusababisha biashara mpya kujitokeza na kuajiri ama kutumika kama ajira binafsi kwa msururu wa wafanyabishara wengine (duplication). Hapo juu tumeona kuwa si wafanyabiashara wote ni wajasiriamali, ila wajasirimali wote ni wafanyabiashara. Hii ni kwa sababu mjasiriamali ana sifa za ziada na za kipekee kumshinda mfanyabiashara.

Sifa hizi za ziada za mjasiriamali ni Mbunifu (innovator), kujitegemea (independent), kujiamini (self-confidence), mpangiliaji (organized), muono (vision), sugu (persistent), Tumaini (optimism), commited, mtendaji (action-oriented), mtatuzi wa matatizo (problem solver), kujihusisha na hatari: kutoogopa kupata hasara (risk taker) na anayenyumbulika (flexiblity).

Sifa hizi ni za mjasiriamali aliyekamilika na aghalabu kukuta mfanyabiashara kuwa nazo. Usihofu kama hauna kipaji cha ubunifu, unaweza kuiga mambo mazuri kutoka kwa wabunifu na ukayatumia ili uweze kujikwamua kuchumi.
 
Itaendelea
 
 Unaweza kukomenti kwenye hii blog :

 Ama niandikie maboresho kwenye mmlanzi@yahoo.com
 

No comments:

Post a Comment