Pages

Monday, September 24, 2012

Wamasai na Waarusha watwangana Arusha...


Chanzo kimoja cha habari kinaarifu kuwa wamasai na waarusha wanapigana kugombea eneo huko oldonyasambo, ambapo ndani ya eneo hilo kuna shule, hivyo wanafunzi wameshindwa kutoka madarasani kutokana na mapigano hayo.

Habari zinaendelea kusema kuwa shule hiyo ndiyo chanzo cha ugomvi huo baada ya kila upande kusema ndiyo wamiliki halali wa shule hiyo hiyo.

Chanzo hicho kimesema kuwa,Polisi na FFU wameshindwa kuwaamulia,mapigano bado yanaendelea mpaka sasa.

Source: Jamii forum

No comments:

Post a Comment