Pages

Sunday, August 19, 2012

Salamu za Eid Mubarak kutoka Kwa Rais Kikwete


Nawatakia sikukuu njema ya Eid (waumini wote wa dini ya Kiislam) na mapumziko mema kwenu nyote. Ramadhani umekuwa mwezi wa shukrani, toba na kuwa pamoja zaidi katika kushirikishana yale tuliyojaaliwa na Mwenyezi Mungu ili kutengeneza jamii bora zaidi. Tuisherehekee sikukuu na mapumziko haya kwa upendo, amani, utulivu na tafakari na baadaye tuendelee vyema na ujenzi wa Taifa letu. Mwisho, Tushiriki kwa pamoja zoezi la sensa siku ya Jumapili tarehe 26/08/2012. Sensa kwa maendeleo. Jiandae kuhesabiwa. Eid Mubarak.

Source: twitter/facebook

No comments:

Post a Comment