Pages

Monday, October 22, 2012

ZIARA YA KIMAFUNZO NARUNYU (MAELEZO NA PICHA)

Jumatatu tarehe 22/10/2012, tumekuwa na ziara ya kimafunzo kwa wakurufunzi wa ngazi ya cheti mkondo A, safari hii ilihusisha walimu watatu ambao walifundisha somo la Principal of Agricultura Technology and dissemination na mmoja aliyeambatana nasi kama mlezi.

Walimu hao ni Lucas Chihwalo, Mgeni Shomari pamoja na Mkali Mlanzi, Mwalimu mkude aliambatana na walimu hao kama Mlezi. Wanafunzi walijifunza mambo mengi ikiwamo aina ya ng’ombe wa maziwa waliopo katika kituo cha masista Narunyu. Tulipokelewa vizuri na wageni wetu ambao ni sista Editha Mbunda na Diana Millanzi ambao ndio walikuwa waelekezaji wakuu.

Masista hawa walituonesha mashine inayotumika kukata kata majani yanayotumika kulishia mifugo (chopping Machine). Mashine hiyo ina uwezo wa kukata kata majani na kuwa madogo kabisa hivyo kumuwezesha ng’ombe kula kiurahisi.

Kwa upande wa mifugo tumejionea aina mbili ya Ng’ombe wa maziwa ambao ni jess ambao wana rangi aina ya dark red pamoja na fresian wenye mabaka meusi na meupe. Katika aina hizi mbili fresian ndio hutoa maziwa kwa wingi ukilinganisha na aina nyingine. Kuna changamoto kadhaa zinazofanya mifugo hii isitoe maziwa kwa wingi ama zinazo zoretesha afya za mifugo hii. Mifugo hii huathiriwa kwa kiwango kikubwa na Tsetse fly wanaosababisha ugonjwa wa Typanasimiosis, na kupe wengine wanaosababisha ugonjwa wa ECF. Njia zinazotumika kuzuia magonjwa haya ni njia ya kuosha mifugo hiyo mara kwa mara kwenye josho kubwa lililopo kituoni hapo. Aidha kuna sista ambaye ana elimu ya kutibu mifugo hivyo hutibu mifugo hiyo mara isumbuliwapo na magonjwa hayo.

Kuna karakana kubwa iliyokuwa inatumika kuzalishia umeme kwa kutumia kinyesi cha ng’ombe (biogas) zamani. Wanafunzi walijionea jinsi kinyesi cha ng’ombe kinavyoweza kutumika kuzalisha umeme kwa mafanikio.

Miradi mingine inayopatikana katika kituo hiki ni kuku wa nyama pamoja na shamba kubwa la miwa, mpunga ndizi pamoja na bustani. Wanafunzi wamejifunza mengi ambayo hayapatikani katika chuo chetu, ni muhimu kwa safari hizi kufanyika kwani huwaongezea ujuzi na uzoefu wanafunzi wetu ambao kwa muda mwingi huwa wanajifunza kinadharia tu na si kivitendo.

Nawasilisha wadau.




 
 


No comments:

Post a Comment