Pages

Friday, August 31, 2012

Bashe, Kigwangallah katika vita ya bastola


BASHE AMTUHUMU KIGWANGALLAH KUMTISHA KWA SILAHA,NAYE AENDA POLISI KUWATUHUMU WAFUASI WA BASHE KUMTISHA


Waandishi Wetu

VITA ya mahasimu wa siku nyingi katika siasa wilayani Nzega, Hussein Bashe na Dk Hamis Kigwangallah imechukua sura mpya, baada ya makada hao wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kufikia hatua ya kutishiana kwa bastola hadharani.Hata hivyo, pamoja na taarifa hizo kuthibitishwa na viongozi wa CCM wilayani humo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Bashe na Kigwangallah kwa nyakati tofauti kila mmoja amekanusha madai hayo akimtuhumu mwenzake kuwa ndiye aliyekuwa na silaha.



Wakati Bashe akisema Dk Kigwangallah ambaye pia ni mbunge wa Nzega ndiye aliyetoa bastola kumstishia wakiwa ndani ya ofisi ya ya CCM Wilaya, Dk Kigwangallah anaeleza kuwa walinzi wa Bashe ndio waliomtishia yeye bastola na kwamba tayari amelifikisha suala hilo polisi ambao wanalifanyia kazi.



Habari zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa, Dk Kigwangallah na Bashe walizua tafrani hiyo juzi wakati wakirejesha fomu za kuwania nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (Nec) kupitia Wilaya ya Nzega.



Upinzani baina ya wanasiasa hao vijana, ulianza 2010 baada ya Kigwangallah kupitishwa na CCM kugombea ubunge katika jimbo hilo licha ya kushika nafasi ya tatu katika kura za maoni, ndani ya chama hicho.



Bashe ambaye aliibuka kidedea katika mchakato huo wa kura za maoni alitoswa na chama hicho kwa maelezo kuwa hakuwa raia wa Tanzania, huku aliyeshika nafasi ya pili, Lucas Selelii ambaye alikuwa kinara wa kupambana na mafisadi wa chama hicho naye akitoswa. Baadaye Waziri wa Mambo ya Ndani wa wakati huo, Lawrence Masha alisema Bashe alikuwa raia halali wa Tanzania.



Vita hiyo ilionekana kuendelea juzi baada ya kudaiwa kutishiana bastola huku kila mmoja akitoa maelezo ya kumrushia lawama mwenzake.



Ilivyokuwa

Katibu wa CCM Wilaya ya Nzega, Kajoro Vyehoroka alisema Bashe alifika ofisini hapo kurejesha fomu saa 09:50 alasiri, muda mfupi baada ya Dk Kigwangallah ambaye alifika saa 09:48.



“Kigwangala alifika na kuingia ofisi ya Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Fransis Shija, ambako alikaa na kujaza fomu yake. Bashe naye alifika akaingia ofisini kwangu, akakaa na kuandika," alisema.



Katibu huyo aliendelea kueleza kuwa ilipofika saa 9:55, Dk Kigwangallah alikwenda kwa katibu muhutasi kurejesha fomu yake na kukaa hapo.



"Bashe alipofika hapo naye alisimama akingoja Kigwangallah amalize, lakini Kigwangallah alimueleza kuwa muda wa kurejesha fomu umemalizika, hivyo kumzuia kurudisha fomu, hali iliyozua mvutano na vurugu" alieleza katibu huyo.



Katibu wa Vijana wa CCM Wilayani Nzega, Salome Nyombi, alisema baada ya vurugu hizo kuzuiliwa ndani ya ofisi ya katibu, Bashe alitolewa nje ambako alianza kuwasimulia rafiki zake kilichotokea ndani.



Alisema baadaye Kigwangallah naye alifika eneo hilo na kuanza kurusha maneno, hali iliyozua mtafaruku mwingine katika eneo hilo.



"Alipozuiliwa kufanya vurugu, aliendelea kutukana na kisha kutoa bastola akiwatishia watu waliokuwa wakizungumza na Bashe kwa madai kuwa ni vibaraka wake," alisema na kuongeza:



“Hali ilikuwa mbaya kiasi cha baadhi yetu kulazimika kukimbia, na wengine tulilala kwenye viti, lakini kijana mmoja anayeitwa Sango, alimzuia (Kigwangallah) kwa kujaribu kumpiga kwa kiti, ndipo watu walipomtoa Bashe na kumpeleka eneo lingine.”



Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wilayani Nzega, Mary Igogo, alisema amesikitishwa na vurugu hizo na kusema iwapo wasingemzuia Bashe, kungezuka ugomvi mkubwa.



Katibu CCM mkoa

Katibu CCM Mkoa wa Tabora, Iddi Ame akizungumuza kwa simu, alisema ndani ya CCM ni ajabu kwa wanachama kutishina kwa silaha.



Ame alisema kuwa kitendo hicho ni aibu kubwa kwa CCM huku akiuagiza uongozi wa Wilaya ya Nzega kutoa maamuzi mapema juu ya vurugu za makada hao.



“CCM hatuna historia ya kutishana kwa bastola na kamwe jambo hilo haliwezi kuwa siasa kwa kuwa linaleta sura mbaya ndani ya chama chetu, nawaagiza uongozi wa wilaya watoe tamko au maamuzi ya jambo hili mapema,”Ame.



Shuhuda

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo ambaye jina lake halikufahamika mara moja, alisema vurugu zilikuwa kubwa zaidi nje ya ofisi za CCM baada ya mahasimu hao kutolewa ndani ya ofisi hizo baada ya kuanza kulumbana.



Taarifa kutoka Jeshi la Polisi zilieleza kuwa Kigwangallah alifika katika kituo cha polisi na kufungua malalamiko ya kutishiwa maisha na Sango Issaya, Hussein Bashe pamoja na Majaliwa Bilali.



Taarifa hizo zilifafanua kwamba kwa nyakati tofauti mahasimu hao walitoa maelezo yao polisi na wapo nje kwa dhamana mpaka pale upelelezi wa tuhuma walizopeana utakapokamilika.



"Tumepokea taarifa za hawa watu na tunaendelea na upelelezi wetu mpaka hapo tutakapojiridhisha na ushahidi ndipo tutawapeleka mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili,”alisema ofisa mmoja wa polisi wa ngazi za juu wilaya.



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Antony Rutta, aliliambia gazeti hili kuwa taarifa za tukio hilo alizipata, lakini anaendelea kuzifuatilia kujua chanzo chake.



“Ni kweli nimepata taarifa za Bashe na Kigwangallah wamedaiwa kutishiana bastola…mimi nilisikia hayo nikiwa njiani kutoka huko Nzega kurudi Tabora….nitafuatilia,”alisema.



Kauli za Bashe, Kigwangallah

Bashe alikiri kutokea vurugu hizo, lakini akakanusha kumtishia bastola Dk Kigwangallah akidai kuwa mwenzake huyo ndiye aliyemtishia yeye kwa bastola akitaka fomu yake isipokelewe kwa kile alichoeleza kuwa imechelewa kurejeshwa.



“Huyu ndugu yangu ana visa na chuki dhidi yangu, ni kweli alinichomolea bastola, lakini wanachama walituamulia," alisema



Hata hivyo, Bashe alieleza kuwa pamoja na hila hizo, Dk Kigwangallah hamuwezi kisiasa kwani katika chaguzi zote zilizowahi kufanyika zikiwahusisha wao, amekuwa akimshinda kwa kishindo.



"Kigwangallah pia aliwahi kuvamia mkutano wangu, lakini niliwaambia watu wangu wamwache. Anachotafuta ni confrontation (msuguano) na mimi ili kutokee tatizo nienguliwe kwenye uchaguzi baada ya kuona haniwezi," alisema.



Bashe alisema kwamba amegundua Kigwangallah anatumia mbinu ili majina yao yakatwe yote kwa kuwa ameshaona hawezi kumshinda. “Jamani Kigwangallah hawezi kunishinda, amenitishia na bastola nikakaa kimya, sikupenda kabisa kumjibu maana najua anachotafuta,” alisema



Kwa upande wake, Dk Kigwangallah alisema aliomba Bashe azuiwe kurejesha fomu yake kwa kuwa aliirudisha nje ya muda, lakini alishangaa kuona anafanyiwa vurugu na wafuasi wake.



Alisema alitishiwa maisha na watu watatu ambao aliwataja akiwamo Bashe na kueleza kuwa tayari malalamiko hayo ameyafikisha polisi.



"Walinzi wa Bashe ndio walionitishia bastola na baada ya tukio hilo nikaenda kuripoti polisi na tayari polisi wamechukua hatua ikiwamo kuwafikisha mahakamani Bashe na wapambe wake hao," alisema Dk Kigwangallah na kuongeza;



“Huyu ndugu yangu (Bashe) ni mzushi anataka kuyakuza mambo tu. Katika hilo Katibu amembeba kwani muda wa kurejesha fomu ulikuwa umeisha".

Alisema Bashe amekuwa akijaribu kumfanyia faulo ya kumtishia huku akitembea na jopo la waandishi wa habari ili wamchafue.



’’Nimeamua kuja kutoa taarifa kwani nimetishiwa maisha yangu na kijana huyu pamoja na Bashe lazima nitoe taarifa hizi, maana nimeonewa,’’alisema Kigwangallah.



Alipoulizwa kana anamiliki bastola, Kigwangallah alisema kuwa kwa muda mrefu amekuwa akimiliki silaha hiyo.



“Kama ningeamua kuua ningeweza kufanya hivyo ila naelewa maana ya kuwa na silaha ya moto, ndio maana nimekuja hapa kutoa taarifa kwa sababu lolote linaweza kutokea” alisema mbunge huyo wakati akiwa Kituo cha Polisi Nzega.



Zungu amkacha Mkono

Katika hatua nyingine mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu ameshindwa kurudisha fomu ya kuwania nafasi ya uenyekiti wa Wazazi Taifa.



Siku ya mwisho ya kurejesha fomu ilikuwa juzi, lakini mbunge huyo ambaye pia ni mwenyekiti wa Bunge alishindwa kuirejesha kama walivyofanya wagombea wengine 16 akiwemo Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono.



Hastin Liumba, Frederick Katukanda, Nzega, Daniel Mjema, Moshi na Joseph Zablon, Dar

Source: Mwananchi

Dk Slaa amvutia pumzi Samuel Sitta


Mwandishi Wetu


KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, amesema kauli iliyotolewa na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ni nzito, hivyo anajipanga kuijibu.
Dk Slaa aliliambia gazeti hili jana kuwa asingependa kuzungumzia kauli hiyo sasa kwa kuwa yuko ziarani vijijini, lakini ataitolea tamko wakati mwafaka ukifika.Habari ambazo baadaye gazeti hili lilizitapa zinasema kuwa Dk Slaa huenda akamjibu Sitta leo, atakapokutana na waandishi wa habari mjini Iringa.

 
Dk Slaa mwenyewe jana jioni alithibitisha kwamba atakutana na waandishi wa habari leo mjini Iringa, lakini hakuwa tayari kueleza kama atazungumzia kauli ya Sitta au la.

 
Kauli ya Dk Slaa imekuja baada ya gazeti hili kumtaka azungumzie kauli ya Sitta kuwa muda wa Chadema kutawala nchi bado, kwa kuwa chama hicho hakina viongozi makini wa kufanya kazi za Serikali.

 
Akizungumza kwa simu na gazeti hili jana Dk Slaa alisema,"Nimemsikia, lakini sijamwelewa. Naomba nipate muda wa kusoma vizuri alichosema, halafu nitamjibu tu."

 
Aliendelea:"Mimi sasa nipo huku Mufindi, sina mawasiliano yoyote ya msingi, naomba nipate muda zaidi wa kujiridhisha maneno yake kabla sijamjibu, nikiwa tayari nitawajulisha (waandishi).”
Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene akizungumza na gazeti hili jana alisema mkutano wa Dk Slaa na waandishi wa habari utalenga kueleza jinsi Chadema kinavyoendesha Operesheni Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), baada ya kuzuiwa kwa mikutano yake ya hadhara.

“Kwenye mkutano na wanahabari, mambo mengi yanaweza kutokea. Kwa hiyo siwezi kukujibu moja kwa moja kama hilo unaloulizia (kauli ya Sitta) nalo litajibiwa au la,”alisema Makene.

 
Sitta alipokuwa akizungumza na baadhi ya viongozi wa CCM wa wilayani Karagwe Mkoa wa Kagera juzi, alisema kuna upungufu mwingi katika safu ya uongozi ya Chadema, kutokana na kutokuwa na watu wenye uzoefu wa kufanya kazi za Serikali, badala yake wana baadhi ya watu wenye uzoefu wa kuongoza kumbi za muziki.

 
Sitta alisema ukimwondoa Dk Slaa, hakuna kiongozi mwingine anayeweza kufanya kazi ya kukiongoza na kukifanya chama hicho kikubalike kwa umma.
“Hawa jamaa hawana hazina ya viongozi kama tulionayo CCM, ambapo tunaweza kusimamisha wagombea 20 wa urais wenye sifa zinazofanana tofauti na wao wanae Dk Slaa tu ambaye inasemekana aliukimbia upadri,” alisema Siita na kuongeza:

 
“Wote hapa mnasikiaga kwamba Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe ni mjuzi wa disko za usiku, sasa huwezi kulinganisha na CCM hata akitoka mtu mmoja chama chetu hakiwezi kuyumba.”
Kuhusu M4C
Katika hatua nyingine, Dk Slaa alizungumzia Operesheni inayojulikana kama M4C akisema Chadema imewabwaga polisi, kutokana na chama hicho sasa kubuni mbinu nyingine ya kujiendesha.
"Tuko huko Mufindi tunajenga chama, vikao kila wakati," alisema Dk Slaa alipoulizwa yuko wapi na anafanya nini.
Dk Slaa alisema CCM na Serikali yake, itajuta kuzuia mikutano ya hadhara ya Chadema kwani baada ya uamuzi huo, chama hicho kimekuja na njia nyingine ya kujijenga maeneo ya vijijini.
"Hawa watajuta (CCM na Serikali) kuzuia mikutano yetu. Sisi tumekuja na njia nyingine ya kukijenga chama vijijini," alisema Dk Slaa ambaye hata hivyo, hakubainisha njia gani anayotumia sasa kukijenga chama hicho cha upinzani.
Alipoulizwa atamaliza lini ziara yake hiyo ya kukijenga chama kwa njia mbadala, alijibu," Tulipanga kutumia siku 44 katika mikoa mitano, lakini nadhani siku hizo zitaongezeka baada ya mikutano yetu kuzuiwa.”
Mwanzoni mwa mwezi huu, Chadema kilianza ziara ya kutembelea maeneo mbalimbali nchini katika kile wanachokiita Movement for Change (M4C).
Hata hivyo, wakiwa mkoani Morogoro, chama hicho kiliingia katika mgongano na polisi katika vurugu zilizosababisha kifo cha mfuasi wake mmoja na majeruhi wawili.
Baadaye Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Said Mwema aliipiga marufuku mikutano na maandamano ya chama hicho iliyopangwa kufanyika mkoani Iringa kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kupisha Sensa ya Watu na Makazi.



Source: Mwananchi

Thursday, August 30, 2012

Taarifa

Hii ni kuwaatarifu kuwa, blog yenu muipendayo itaendelea kutoa taarifa mbalimbali kama kawaida na siku za mapumziko, nitakuwa nawaletea taarifa za michezo na burudani kutoka katika vyanzo mbali mbali vya habari.


Karibu tuendelee kupashana Habari

Sitta: Tishio Chadema ni Dk Slaa tu

ADAI WENGINE NI WAZOEFU WA KUONGOZA KUMBI ZA MUZIKI, ATAMBA CCM KINA ZAIDI YA WATU 20 WENYE SIFA ZA URAIS, ZITTO AMJIBU


Edwin Mjwahuzi, Karagwe

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya CCM, Samuel Sitta amekiponda Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), akidai kuwa muda wake wa kutawala nchi bado, kwa kuwa hakina viongozi wa kutosha wa kufanya kazi za Serikali ukimwondoa Katibu Mkuu wake, Dk Willibrod Slaa.


Sitta ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na baadhi ya viongozi wa CCM wa Wilaya ya Karagwe, Kagera, alikokuwa katika ziara ya kutembelea ofisi za CCM.


Alisema kuna upungufu mwingi katika safu ya uongozi wa chama hicho, kutokana na kutokuwa na watu wenye uzoefu wa kufanya kazi za Serikali, badala yake akidai kuwa kina baadhi ya viongozi wenye uzoefu wa kuongoza kumbi za muziki.Wote hapa mnasikia kwamba Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe ni mjuzi wa disko za usiku, sasa huwezi kulinganisha na CCM hata akitoka mtu mmoja chama chetu hakiwezi kuyumba.


Dk Slaa na Mbowe hawakupatikana jana kuzungumzia kauli hiyo ya Sitta baada ya taarifa kueleza kuwa Mbowe yuko nje ya nchi na alikuwa hapatikani kupitia simu yake ya mkononi kama ilivyokuwa kwa Dk Slaa.


Hata hivyo, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe alipinga kauli hiyo akimtaka Sitta aachane na chama hicho kikuu cha upinzani na atumie muda wake kukijenga chama chake ambacho alidai kuwa kina makundi zaidi ya sita.


Mwaka 2005 tuliweka mgombea Mbowe, mwaka 2010 tukamweka Dk Slaa, mwaka 2015 anaweza akarudi Mbowe, Dk Slaa au mwanachama yeyote wa Chadema, alisema Zitto.


Alisema Chadema ni taasisi na si chama cha makundi kama ilivyo kwa CCM hivyo hakiwezi kumtegemea mtu mmoja..Sitta asigombane na Chadema, ajenge chama chake ili tukutane mwaka 2015.


Akizungumza na viongozi hao wa CCM Karagwe, Sitta alisema hakuna kiongozi mwingine anayeweza kufanya kazi ya kukiongoza Chadema na kukifanya chama kikubalike kwa umma.


Hawa jamaa hawana hazina ya viongozi kama tulionayo CCM, ambapo tunaweza kusimamisha wagombea 20 wa urais wenye sifa zinazofanana tofauti na wao wanaye Dk Slaa tu ambaye inasemekana aliukimbia upadri.


Kuhusu CCM

Akizungumzia chama chake, Sitta aliwataka viongozi wa CCM Mkoa wa Kagera kutokaa kimya na badala yake wajitoe na kujibu hoja za upinzani wanazozitoa kuikosoa Serikali iliyopo madarakani ili ionekane haijafanya mambo ya maendeleo tangu kupatikana kwa uhuru.


Serikali ya CCM imefanikiwa katika maeneo mengi ya huduma za jamii kama elimu, barabara, afya na mawasiliano, sasa inashangaza kuona viongozi wa chama mnashindwa kufanya mikutano ya kuwaeleza wananchi mafanikio yanayotokana na utekelezaji wa sera na ilani ya chama chetu.


Sitta aliwataka viongozi chama hicho nchini kuepuka mapambano na chuki miongoni mwao lakini akasisitiza kwamba kinaendelea na mkakati wake wa kuwaondoa viongozi wanaodaiwa kuwa ni mafisadi maarufu kwa jina la magamba.

Alisema chuki na mapambano yanayoendelea ndani ya chama hicho ndiyo yanayochangia kukidhoofisha na kuwapa la kusema wapinzani na hata kusababisha baadhi ya wanachama kukihama.


Mapambano ndani ya CCM ndiyo chanzo cha migogoro na mitafaruku inayosababisha viongozi na wanachama wetu kuombeana mambo mabaya na kutoa mwanya kwa watu wetu kuhamia upinzani.


Sitta yupo katika ziara ya siku tano ya kiserikali mkoani Kagera kukagua miradi mbalimbali inayohusiana na mwingiliano wa uchumi na kijamii kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Source: Mwananchi

Sunday, August 26, 2012

Chadema yatingisha Igunga

YAFANYA MKUTANO MKUBWA IGUNGA KUSHUKURU WAPIGAKURA,DK SLAA AIONYA CCM IKIKATA RUFAA ITAUMBUKA

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana kilitikisa Jimbo la Igunga mkoani Tabora, kwa kufanya mkutano mkubwa wa hadhara ikiwa ni mara ya kwanza tangu Mahakama Kuu Kanda Tabora kutengua ubunge wa Dk Dalaly Kafumu wa Chama Cha Mapinduzi, huku kikiionya CCM kuwa kitaumbuka iwapo kitakata rufaa kwa uamuzi huo wa mahakama.

Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika katika Viwanja vya Sokoine, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa alisema CCM kisithubutu kukata rufaa kwani kitaumbuka kwa kuwa kilicheza faulo nyingi katika uchaguzi huo.

Alisema ameshangazwa na kauli ya CCM kusema kuwa kitakata rufaa katika kesi hiyo wakati kisheria, kwa kesi za uchaguzi na pia katika hatua hiyo chama hakina nafasi yoyote bali mgombea au mwanachama wa chama husika, ndiye anayeweza kwenda mahakamani kufungua kesi na kupinga.

Katika mkutano huo uliofurika maelfu ya wanachama na washabiki wa wa chama hicho, Dk Slaa alisema kuwa Chadema kitakiangusha vibaya CCM hata ikiwa uchaguzi katika Jimbo la Igunga utarudiwa.

Huku akitoa mifano mbalimbali ya jinsi baadhi ya wanachama wa CCM walivyokuwa wakitoa rushwa, Dk Slaa alimtuhumu Mweka Hazina wa chama hicho, Mwigulu Nchemba, ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi kwamba alikuwa kinara wa kutoa rushwa katika kampeni za uchaguzi mdogo wa Igunga Oktoba mwaka uliopita.

“Chadema imejipanga kwa rufaa hiyo ya CCM ikiwa ni pamoja na kufungua kesi nyingine dhidi ya vigogo wa CCM, walioshiriki katika kampeni za uchaguzi huo,”alisema Dk Slaa.

Dk Slaa pia alimponda Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama akieleza kuwa mdomo wake umemponza kwa sababu alikuwa akizungumza mambo ambayo hakujua madhara yake.

Wakati akitoa hukumu ya kesi hiyo, Jaji Mary Nsimbo Shangali wa Mahakama Kuu alisema moja ya hoja saba zilizotolewa na Chadema ambayo mahakama iliikubali ni ile ya Mukama kudai Chadema kilipeleka makomandoo katika uchaguzi huo na kupanga kuuvuruga.

Dk Slaa alisema: “Mukama alikurupuka kwa kutamka maneno bila kufanya utafiti hali iliyosababisha CCM kupoteza jimbo.”

Alikwenda mbali zaidi na kueleza kuwa suala la CCM kuingiza silaha ndani ya nchi, bila kibali wala leseni na kuwapatia vijana wake mafunzo katika kambi za Ilemo, Iramba mkoani Singida linamhusu mwenyekiti wa chama hicho na siyo mtu mwingine.

Alidai kuwa wakati wa uchaguzi wa Igunga, vijana hao walikuwa wakipewa mafunzo ya kijeshi akisisitiza kuwa suala hilo linamhusu mwenyekiti wa chama hicho akimtaka atoe majibu na ufafanuzi juu ya hilo.

Dk Slaa alisema kuwa siku ya jana ilikuwa ni kwa ajili ya wananchi wa Igunga kusherehekea na kupongezana kwa mshikamano waliouonyesha wakati wote wa kusikilizwa kwa kesi hiyo, huku akitoa pongezi kwa mawakili waliosimamia kesi hiyo kwa kuiwakilisha vyema Chadema katika kesi hiyo.

Naye upande wake aliyekuwa mgombea wa Chadema katika uchaguzi mdogo wa Igunga Oktoba mwaka uliopita, Joseph Kashindye aliwashukuru wananchi walioiunga mkono Chadema akieleza kuwa wameonyesha ushirikiano mkubwa uliokipa ushindi chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Kashindye aliwashukuru pia wananchi wa Igunga kwa kukichangia Chadema Sh6 milioni zilizosaidia kulipia gharama za kesi hiyo pamoja na malazi kwa mashahidi mbalimbali waliotoa ushahidi kwenye kesi dhidi ya CCM iliyotolewa hukumu wiki iliyopita kwa kutengua ushindi wa Dk Dalaly Kafumu wa CCM.

“Mahakama imetenda haki kwa kuwa imetoa hukumu ya haki…, nimeamini kuwa haki ya mtu haipotei. Awali nilidhani kuwa mahakama ni mali ya CCM kumbe si kweli,” alisema Kashindye na kushangiliwa na mamia ya watu waliofurika katika uwanja huo.

Kashindye aliponda ahadi zilizokuwa zikitolewa na Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa kwamba ndizo zilizofanya CCM kushindwa kesi.

“Watu wa ajabu sana, wametoa ahadi za kujenga madaraja, kusaidia chakula wakati hilo ni jukumu la Serikali,” alisema Kashindye akionyesha kushangaa.

Alibainisha kuwa wakati kesi hiyo ikinguruma mahakamani, alikuwa akitafutwa na wanachama wa CCM, lakini kutokana na kujua mbinu zao, aliamua kujichimbia kusikojulikana.

Dk Kafumu aliibuka mshindi katika uchaguzi huo mdogo uliofanyika Oktoba 2, mwaka jana kuziba nafasi ya Rostam Aziz ambaye alijiuzulu kwa madai kwamba anaachana na siasa chafu ndani ya CCM.

Katika uchaguzi huo kulikuwa na upinzani mkubwa kati ya Dk Kafumu na aliyekuwa mgombea wa Chadema, Joseph Kashindye ambaye hakuridhishwa na mwenendo wa uchaguzi huo, hivyo kuamua kupinga matokeo hayo mahakamani. Kesi hiyo ilifunguliwa Machi 26, mwaka huu.
 
Source: Mwananchi

Thursday, August 23, 2012

Chenge kumtetea Mramba kesi ya ufisadi


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, kesho itaanza kusikiliza utetezi wa kesi ya matumizi mabaya ya ofisi na kuisababishia serikali hasara ya Sh. Bilioni 11.7, inayomkabili mawaziri wa zamani, Basil Mramba, Daniel Yona na Katibu mkuu wa Hazina, Gray Mgonja baada ya kukutwa wana kesi ya kujibu.

Utetezi huo utasikilizwa mbele ya jopo la mahakimu watatu wakiongozwa na Jaji John Utamwa na Sam Rumanyika wa Mahakama Kuu waliopewa kibali na Jaji Mkuu kuendelea kusikiliza kesi hiyo wakisaidiana na Saul Kinemela.

Upande wa Mashtaka unaongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi Osward Tibabyekomya akisaidiana na Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kupambana na Kuzia Rushwa (Takukuru), Ben Linkolin.

Upande wa utetezi unawakilishwa na mawakili, Herbat Nyange, Cathbert Tenga na Elisa Msuya.
Mapema mahakama hapo bila kuacha shaka iliwaona washtakiwa wana kesi ya kujibu baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na pande zote mbili.

Awali mahakamani hiyo, upande wa mashtaka ulifunga ushahidi wake baada ya kuita mashahidi 13 na kuwasilisha vielelezo 26 mahakamani.

Katika kesi ya msingi, washitakiwa wanadaiwa kuwa, kati ya Agosti mwaka 2002 na Juni 14 mwaka 2004 jijini Dar es Salaam, wakiwa watumishi wa umma kama mawaziri na katibu mkuu walitumia vibaya madaraka.

Ilidaiwa kuwa kwa kupitia kampuni ya Alex Stewart (ASSAYERS) ya Uingereza iliyoingia mkataba wa ukaguzi wa madini ambapo kwa kupitia kampuni tanzu ya Alex Stewart (ASSAYERS) Government Business Corporation waliingia mkataba kukagua kiwango cha uzalishaji wa madini ya dhahabu kinyume cha Sheria ya Manunuzi ya Umma.

CHANZO: NIPASHE

Wednesday, August 22, 2012

Dovutwa amfananisha Lowassa na Kawawa

Mh Lowasa.
MWENYEKITI wa Chama cha United Peoples Democratic (UPDP), Fahmi Dovutwa, amemfananisha Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa na Waziri Mkuu Mstaafu, marehemu Rashid Kawawa.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Dovutwa alisema Lowassa hana tofauti na Kawawa, ambaye katika uhai wake akiwa waziri mkuu alibeba lawama za Serikali katika utawala wa awamu ya kwanza.

Dovutwa ambaye mwaka 2010 aligombea urais, alisema Lowassa hakuhusika katika kashfa ya rushwa iliyotokana na mkataba tata wa Richmond na kwamba alijiuzulu uwaziri mkuu ili kulinda heshima ya Serikali na si vinginevyo.

“Mwalimu Nyerere alipata kutoa hotuba siku moja akisema kwamba: ‘Namshukuru sana mzee Rashidi Mfaume Kawawa, amenisaidia sana.

‘Mambo yote ambayo amekuwa akilaumiwa Kawawa niliyafanya mimi na yeye (Kawawa) alibeba tuhuma hizo kwa ajili yangu’, haya ni maneno ya Baba wa Taifa na hotuba zake hizi zipo,” alisema Dovutwa akimnukuu Mwalimu.

Dovutwa aliongeza: “Kwa kauli hiyo ya Baba wa Taifa ni wazi Lowassa hakuhusika na kashfa ya Richmond. Kwa sababu maamuzi ya kiutendaji wa Serikali yako mikononi mwa Baraza la Mawaziri ambalo mwenyekiti wake ni Rais.

“Waziri yeyote hana uwezo wala mamlaka ya kuamua jambo bila ridhaa ya Rais. Lowassa aliwajibika ili kuilinda Serikali ya CCM chini ya Rais Kikwete isianguke na kupisha uchaguzi mwingine,” alisema.

“Mwalimu Nyerere alielewa vizuri dhana ya uwajibikaji na Watanzania wengi hawakumwelewa Mwalimu Nyerere alipokuwa akiwarudisha baadhi ya watumishi ambao awali waliwajibika kwa tuhuma za kiutumishi.

“Kimsingi tuhuma alizokuwa amelaumiwa kiongozi mwandamizi wa Serikali zilikuwa ni tuhuma za kiongozi mkuu wa Serikali ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kuamua kufanya jambo au kulikataa.

“Ili kuilinda Serikali na kiongozi mkuu wa Serikali ndipo hutokea mtumishi mmoja wa Serikali kubeba lawama na tuhuma za wizara yake kwa manufaa ya Serikali yenyewe.

Hivyo dhana ya kuwajibika ilieleweka vizuri kwa Mwalimu Nyerere kuliko wasomi walio wengi wa ndani na nje ya CCM,” alisema Dovutwa.

Dovutwa alisema Lowassa ni kiongozi makini mwenye ujasiri ambaye aliweza kufanya mambo akiwa waziri mkuu, huku akiwatahadharisha wananchi kuwa makini na baadhi ya viongozi.

“Watanzania tusikumbuke kufanya mabadiliko ambayo huenda tukaondoa wala rushwa wadogo na kuingiza wala rushwa wakubwa zaidi,” alisema.

Dovutwa aliwataka Watanzania kutafakari juu ya mwenendo wa vyama vilivyoko bungeni, hasa kutokana na Bunge kuchafuka kutokana na kashfa ya rushwa inayowahusisha wabunge.


Source:www.jamiiforum.com

CCM, Rage mficha ugonjwa mwisho huumbuliwa hadharani

Vyombo vya dola, serikali na CCM walifanya jitihada za ziada kuzima kashfa ya Rage kupanda na silaha kali hadharani wakati wa kampeni huko Igunga. Kwa bahati wanaotegemea nguvu ya Mungu hulindwa pale bila Rage kujua shati lake limefunuliwaje hadi wenye uchu wa kutopitwa na taswiras za matukio kunasa picha kwa nafasi nzuri isiyo na utata.

Polisi, Maofisa wasimamizi wa kampeni na uchaguzi, serikali na CCM yenyewe kufanya jitihada zisizo za kawaida kufifisha jambo hilo kwa kuudanganya umma kwamba amepata adhabu ya kulipa faini ya Tsh 100, 000. Faini hiyo ilikuwa ni kinyume cha sheria za uchaguzi kwani jambo hilo lingefanyika na chama cha upinzani mambo yangekuwa makubwa.

Hatimaye pamoja na hoja nyingine kadhaa kati ya saba, moja ya hoja nzito ambazo Mahakama Kuu kanda ya Tabora imeegemea kumvua ubunge Dr. Kafumu ni hili la Aden Rage kupanda jukwaani na silaha kali kutishia wapiga kura.

Binafsi napongeza makama za Tanzania kuanza kufunguka na kulinda haki kwa misingi ya kufuata sheria bila kujali sura ya mtu ikoje. Kama mahakama zitazidi kufunguka hivyo itasaidia kujenga utawala wa kisheria ambao kwa sasa unapindishwa kila kukicha na wenye malengo binafsi ya kuhodhi nchi hii kama yao.

Sunday, August 19, 2012

Salamu za Eid Mubarak kutoka Kwa Rais Kikwete


Nawatakia sikukuu njema ya Eid (waumini wote wa dini ya Kiislam) na mapumziko mema kwenu nyote. Ramadhani umekuwa mwezi wa shukrani, toba na kuwa pamoja zaidi katika kushirikishana yale tuliyojaaliwa na Mwenyezi Mungu ili kutengeneza jamii bora zaidi. Tuisherehekee sikukuu na mapumziko haya kwa upendo, amani, utulivu na tafakari na baadaye tuendelee vyema na ujenzi wa Taifa letu. Mwisho, Tushiriki kwa pamoja zoezi la sensa siku ya Jumapili tarehe 26/08/2012. Sensa kwa maendeleo. Jiandae kuhesabiwa. Eid Mubarak.

Source: twitter/facebook

Saturday, August 18, 2012

HATARI:Tanzania President rejects war,Banda insists whole lake belongs to Malawi

                               

By Nyasa Times Reporter












 
Tanzanian President Jakaya Kikwete has categorically denied reports that his country is preparing to go to war with its neighbour, Malawi, because of a dispute over Lake Malawi, where a British- based company is exploring for oil.

Speaking to journalists after a closed discussion with the Malawi President Mrs Joyce Banda in Maputo, Mozambique, the Tanzanian leader said the war mongering comments were coming from overzealous opposition parties in his country who want to score political mileage over the issue.

“I am the Commander of the army. I have not issued any directive to my armed forces for war. So if it did not come from me, it is not true,” said Kikwete.

There have been reports of war by the Tanzanian media that army tanks and forces have been patrolling the Tanzanian side of the lake.

Kikwete said his country has over the years enjoyed good relationship with Malawi and it has no intention to strain it in any way.

Dialogue
The Tanzanian leader who kept on referring to the Malawi President Banda as “my sister said the two countries will use dialogue to resolve the issue.
The two countries have set up a working committee which will meet on August 20 in Mzuzu city, northern Malawi.

President Banda said she is hopeful that the border issue will be handled “diplomatically”.
She thanked President Kikwete for sparing time to discuss the matter, saying it had raised fears among people living along the lake.

 Ownership
President Banda however maintained that the whole lake belongs to Malawi and former Tanzanian leaders including Julius Nyerere and Benjamin Mkapa have both honoured the lake boundaries agreed upon in 1890 and reaffirmed after independence.

“Malawi owns 100 percent of the lake,” she said.
But Banda stressed that her government will continue to engage Tanzania into a diplomatic dialogue to resolve the border dispute amicably.

Since the wrangle began in July following Malawi’s prospecting for oil in Lake Malawi through an international firm, Surestream, there has been speculations of the two countries planning to go to war over who owns the African’s third largest lake.

But President Banda stressed that war between the two countries could never be the solution.
President Kikwete, however, said his government will leave the issue to the working technical committee of the two countries to get to its final conclusion.

 Jokes
Meanwhile, during Southern Africa Development Community (SADC) summit in Mozambique, Zambian President Micheal Sata interjected the chairperson’ speech to joke about the border dispute between Malawi and Tanzania.

When opening the summit earlier, Mozambican President Armando Guebuza said the regional bloc will also have to confront a brewing border conflict between Malawi and Tanzania.
But ut Sata saw an opportunity to joke.
“If they start fighting we are going to host the refugees,” he shouted from his seat.

 Treaty
Malawi government’s stand on the matter is that Lake Malawi entirely belongs to the country as stipulated in the 1890 Heligoland Treaty, also known as Anglo-German Treaty, signed among the United Kingdom of Great Britain, Ireland and German concerning territorial interests in Africa.

According to the Malawi government, the Heligoland Treaty was also reinforced by both the 1963 Treaty and Agreement of the Organization of African Union (OAU) and its successor African Union (AU) in 2002 and 2007 that “member states should recognize and accept the borders that were inherited at the time of independence.”
President Kikwete and President Banda: Cordial relationship

Dk. Ulimboka: Ninayejua ukweli ni mimi...

Dr Ulimboka
HATIMAYE Mwenyekiti wa Jumuiya ya Chama cha Madaktari, Dk. Steven Ulimboka, ameibuka toka mafichoni na kuwaambia Watanzania kwamba anayejua mpango mzima wa kumteka, kumtesa na kumpiga ni yeye pekee.

Dk. Ulimboka ambaye juzi alikuwa mafichoni, alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na gazeti hili kuhusiana na tukio zima la kutekwa, matibabu yake nchini Afrika Kusini na mambo mengine yaliyojiri wakati akiwa nje.

Huku akiwa makini kuchagua maneno, Dk. Ulimboka alisema waandishi wa habari wasiihoji familia yake wala mtu mwingine yeyote, kwani ukweli wa tukio lake anaujua yeye mwenyewe.

Dk. Ulimboka ambaye tangu arejee amekuwa akiishi kwa kujificha, amewataka Watanzania kuvuta subira kwani anajipa muda wa kueleza ukweli wa tukio la kutekwa kwake.

“Najua waandishi wa habari na Watanzania wengi wanataka kujua ukweli ambao ninao mwenyewe, lakini hakuna sababu ya kuwa na haraka, wakati ukifika nitazungumza yaliyonisibu,” alisema.

Hata hivyo, Dk. Ulimboka ambaye alikuwa kiongozi wa mgomo wa madaktari uliolitikisa taifa hivi karibuni, hivi sasa anaishi kwa hofu na kujificha huku akichagua marafiki wa kukutana na kuzungumza nao. Kiongozi huyo, yuko makini pia katika kuzungumza na simu, na amekuwa akipokea zile za watu anaowajua tu.

Alipobanwa ili azungumze kwa ufupi juu ya wanaohusika na kutekwa kwake, Dk. Ulimboka alisisitiza kuwa hayuko tayari kueleza ukweli huo kwa sasa na kuongeza kuwa muda ukifika ataeleza kila kitu.

Polisi wapanga kumhoji

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Polisi Dar es Salaam, Suleiman Kova ametoa kauli inaonesha kwamba vyombo vya usalama vitamuhoji Dk. Ulimboka.

Kova ambaye alikuwa akizungumza na gazeti hili, lililotaka kujua msimamo wa vyombo vya usalama katika kulishughulikia suala la Ulimboka, hasa baada ya kurejea kutoka kwenye matibabu nchini Afrika Kusini, alisema kwamba taratibu za kipelelezi zitafuatwa.

Wakati Kova akizungumza hayo, chanzo kimoja cha habari toka kwa maofisa wa ngazi za juu wa polisi kilidokeza kuwa endapo Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) katika uchunguzi wake atabaini kuwa kuna shahidi muhimu anahitajika, atahojiwa.

Hata hivyo Kova alisisitiza kuwa; “watu wakipeleleza hawasemi ila tambua tu kwamba taratibu za upelelezi zitafuatwa.”

Tayari taarifa na mwenendo wa tukio zima zinaonesha pasipo shaka kuwa, Jeshi la Polisi katika taratibu zake sasa linafikiria kumuita na kumuhoji Dk. Ulimboka ili liweze kuondoa maneno ya kusikia sikia.

Kuhusu kutajwa tajwa kwa mtu anayedaiwa kuwa ni ofisa wa Usalama wa Taifa wa Ikulu, Ramadhan Ingondhur kuwa alihusika na njama za kumteka na kumtesa Dk. Ulimboka, Kova aliahidi kulizungumzia hilo siku ya Ijumaa.

Mbali na gazeti la MwanaHalisi kumtaja Ramadhan kuwa ndiye mhusika mkubwa wa kutekwa kwa Dk. Ulimboka, mwingine aliyeungana na msimamo huo ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa ambaye aliitaka Idara ya Usalama wa Taifa pamoja na serikali ithibitishe hadharani juu ya mtu anayetajwa kuhusika na tukio hilo.

Dk. Slaa alisema chama chake kitaanzisha harakati za kutaka kujua ukweli wa nani anahusika kumteka Dk. Ulimboka. Mwanzoni mwa wiki, Dk. Ulimboka alirejea kwa kishindo nchini kutoka Afrika Kusini alikokuwa anatibiwa, na kusema yupo tayari kuendeleza mapambano na kazi baada ya kupona kabisa. Dk. Ulimboka alikwenda Afrika Kusini Juni 30 mwaka huu kwa ajili ya matibabu baada ya kutekwa, kupigwa na kutelekezwa kwenye msitu wa Pande nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia Juni 27, 2012.

Aliondoka nchini akiwa kwenye kitanda cha wagonjwa kwa vile alikuwa kwenye hali mbaya kiafya, lakini alirejea akitembea kwa miguu na kuonekana mwenye afya njema.


 Source:www.jamiiforum.com

Wednesday, August 15, 2012

Ripoti Maalum: Utetezi wa Tundu Lissu (MB) mbele ya kamati ya Haki na Maadili ya bunge

Mh Lissu

UTANGULIZI
 Julai 13, 2012 Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni iliwasilisha Maoni yake kuhusu Mpango na Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka wa fedha 2012/2013. Pamoja na mambo mengine, Maoni ya Kambi yalihusu utaratibu wa uteuzi wa majaji wa Mahakama ya Tanzania.

Maoni ya Kambi yalizua mjadala mkubwa ndani na nje ya Bunge huku wachangiaji wengi wakimtuhumu Msemaji wa Kambi kwa “kuidhalilisha” Mahakama na/au “kuwadhalilisha majaji” (Gosbert Blandes-Karagwe CCM); “kuwavunjia heshima majaji” (Naibu Spika Job Ndugai); kuwatukana na kuwadhalilisha majaji (Murtaza Mangungu-Kilwa Kaskazini); “kuwa-offend, kuwadhalilisha na kuwanyanyasa majaji” (Assumpter Mshama-Nkenge CCM); “kufedhehesha Mahakama na majaji” (Mwanasheria Mkuu wa Serikali Frederick Werema).

Aidha, Msemaji wa Kambi alishambuliwa kwa kudaiwa kuwa mfitini na asiye na akili timamu (Muhammad Chomboh- Magomeni CCM)); na “kujiamini kwamba yeye anajua zaidi kuliko watu wengine wote” (Mangungu). Kwa upande wake, Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe alilihakikishia Bunge kwamba “... haijatokea hata siku moja katika nchi hii Rais akamteua Jaji wa Mahakama Kuu bila kuzingatia mapendekezo yaliyopelekwa kwake na hii Tume ya Uajiri wa Mahakama.” Zaidi ya hayo, “... labda Mheshimiwa Lissu anamjua Jaji angalau mmoja na anaweza akamtaja aseme Jaji huyu ametolewa tu mitaani na Mheshimiwa Rais, yupi hakuna… hawa majaji wote walioteuliwa wamepitia mchakato huu wa kikao kizito sana cha watu ambao ndiyo wenye sheria ya nchi hii.”

Baadaye Msemaji wa Kambi alitakiwa kufuta kauli yake kuhusu uteuzi wa majaji usiofuata utaratibu uliowekwa na Katiba. Msemaji wa Kambi alikataa kufuta kauli hiyo ambako Mwenyekiti wa Kikao alielekeza Msemaji wa Kambi apelekwe kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa hatua zaidi. Alichukua uamuzi huo ili masuala hayo yapatiwe ufafanuzi ili wananchi wapate picha kamili na ya kweli kuhusu jambo hili muhimu. Maelezo haya yana lengo la kutoa ufafanuzi huo.

Katika maelezo yake kwa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya BUnge, Lissu alisema, “Nitajitahidi kwa kadri inavyowezekana kutoa ushahidi unaothibitisha kwamba siyo tu kwamba utaratibu wa kikatiba katika uteuzi wa majaji umekiukwa mara nyingi, bali pia majaji wengi walioteuliwa kwa utaratibu wa nje ya Katiba wamekuwa hawana ‘uwezo, ujuzi na kwa kila hali hawakufaa kukabidhiwa Madaraka ya Jaji wa Mahakama Kuu.”

TATIZO LA MUDA MREFU

Kuna ushahidi mkubwa kuthibitisha kwamba kuna watu wameteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu “... wakiwa wamekaribia muda wao wa kustaafu kwingineko katika utumishi wa umma (na) wanapewa ‘zawadi’ ya ujaji ili kuwawezesha kupata mafao ya majaji wastaafu ambayo yameboreshwa sana katika miaka ya karibuni.” Ni muhimu kuweka wazi hapa kwamba utamaduni huu haukuanza baada ya Rais Jakaya Kikwete kuchaguliwa kuwa Rais, bali ni tatizo la muda mrefu. Kwa mfano, marehemu Jaji Kulwa Masaba na Jaji Madina Muro na majaji Stephen Ihema, Juxton Mlay, Augustine Shayo na Vincent Lyimo waliteuliwa majaji wa Mahakama Kuu baada ya utumishi wa muda mrefu kwingineko katika utumishi wa umma.

Majaji Masaba na Muro waliteuliwa huku wakiwa wagonjwa mahututi na – kwa kadri ninavyofahamu - hawakuwahi kuandika hukumu hata moja kabla ya mauti kuwafika! Jaji Lyimo aliteuliwa Machi 28, 2007 mwaka mmoja kabla ya muda wake wa kustaafu kwa mujibu wa sheria. Hata hivyo, ilipofika Oktoba 26, 2007 Katibu Mkuu Kiongozi wakati huo Phillemon Luhanjo alimtaarifu Jaji Mkuu kwamba Rais Kikwete “... ameamua kusogeza mbele muda wa kustaafu wa Mheshimiwa Jaji Vincent Kitubio Damian Lyimo kwa miaka mitatu kuanzia Machi 28, 2008 siku ambayo angestaafu kwa lazima”!

Kwa upande wao, Majaji Ihema, Mlay na Shayo walijizolea umaarufu kwa kuwa majaji wasioandika hukumu na hivyo kuwa wacheleweshaji wakubwa wa kesi katika Mahakama Kuu. Jaji Ihema alitia fora kwenye jambo hili kiasi kwamba Juni 16, 2003 Mwenyekiti wa sasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Mzee Joram Allute, alilazimika kumwandikia Rais Benjamin Mkapa maombi ya kumwondoa Jaji Ihema kama Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania “kwa uzembe na kukosa maadili.”

Mzee Allute alikuwa na kesi kwa Jaji Ihema ambapo Jaji huyo ‘alikalia’ uamuzi kwa zaidi ya miaka minne hadi aliponyang’anywa faili la kesi hiyo na kukabidhiwa Jaji mwingine aliyeandika uamuzi ndani ya wiki tatu! Mwezi mmoja kabla ya barua ya Mzee Allute kwa Rais Mkapa, mawakili wake walikuwa wamemwandikia Jaji Mkuu Barnabas Samatta kulalamikia ucheleweshaji wa uamuzi wa kesi hiyo. Mawakili hao walidai: “Hadhi na heshima ya Mahakama inaporomoka vibaya kama inachukua zaidi ya miaka mitatu kwa Jaji kutafakari na kutoa uamuzi kwa jambo jepesi kama maombi ya pingamizi.” Licha ya malalamiko haya dhidi yake, Jaji Ihema alipatiwa mkataba wa ajira wa miaka miwili mara baada ya kustaafu mwaka 2005.

MAJAJI WA MIKATABA

Agosti 2, 2005 Jaji Kiongozi Hamisi Msumi alitoa taarifa kwa majaji wote wa Mahakama Kuu kwamba Jaji Ihema alikuwa amepewa mkataba mpya baada ya kustaafu kama Jaji wa Mahakama Kuu. Taarifa hiyo ilimfanya Jaji Bernard Luanda, wakati huo Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba, kuhoji ‘Uhalali Kikatiba kwa Majaji Kufanya Kazi kwa Mkataba Baada ya Kustaafu.’ Katika taarifa yake kwa Jaji Kiongozi Msumi, Jaji Luanda alisema kwamba “... suala la majaji kupewa mikataba ... linaenda kinyume na Katiba.” Jaji Luanda alifafanua: “Kwa kuwa Jaji amestaafu, basi kiapo chake nacho kimeondoka. Kwa bahati mbaya hawaapishwi ili washike kazi hizo za ujaji.... Ni hoja yangu kwamba Majaji waliostaafu na kupewa mikataba si Majaji kwa mujibu wa Katiba.”

Msimamo wa Jaji Luanda uliungwa mkono mwaka mmoja baadaye na Jaji wa Rufaa, Augustino Ramadhani wakati huo akiwa Kaimu Jaji Mkuu. Katika ‘Mawazo Kuhusu Vifungu Vinavyohusu Mahakama na Majaji’ aliyomwandikia Jaji Mkuu Samatta na kunakiliwa kwa Majaji wa Rufaa wote, Jaji Ramadhani alisema kwamba “... sio sahihi kwa Jaji Mkuu kustaafu na kupewa mkataba wa kuendelea na wadhifa huo kupindukia umri wa miaka 65 (ambao ndio umri wa kustaafu kwa lazima kwa Jaji wa Rufaa na Jaji Mkuu).” Baadaye Jaji Luanda aliteuliwa kuwa Jaji wa Rufaa wakati Jaji Ramadhani alikuja kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

Kauli ya Kambi kwamba kuna ukiukaji mkubwa wa Katiba kuhusiana na uteuzi wa majaji inaungwa mkono na nyaraka za ndani ya Serikali na hasa Ofisi ya Rais, Ikulu yenyewe. Desemba 6, 2007, mkutano kuhusu ajira ya majaji waliostaafu ulifanyika Ikulu, Dar es Salaam chini ya uenyekiti wa Katibu Mkuu Kiongozi Luhanjo. Wajumbe wengine walikuwa pamoja na Mwanasheria Mkuu Johnson Mwanyika na Naibu wake Sazi Salula, Katibu Mkuu Utumishi George Yambesi, Msajili wa Mahakama ya Rufani, Sophia Wambura na Susan Mlawi wa Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri.

Kwa mujibu wa Kumbukumbu za Mkutano huo, “kwa utaratibu unaotumika sasa, baadhi ya Majaji wanaofikisha umri wa kustaafu kwa mujibu wa Ibara ya 110(1) kwa Majaji wa Mahakama Kuu na Ibara ya 120(1) ya Katiba wanaongezewa muda wa kuendelea na utumishi wao kwa mkataba baada ya wao kuwasilisha maombi rasmi.” Baada ya mjadala juu ya jambo hili, wajumbe wa mkutano walikubaliana kwamba “utaratibu wa kuongeza muda kwa njia ya mkataba unakiuka masharti ya Katiba na kuleta mkanganyiko kama Majaji hao wanastahili kulipwa mshahara au pensheni au vyote kwa pamoja.”

Matokeo ya mkutano wa Ikulu ilikuwa ni kuundwa kwa ‘Kikundi Kazi kwa Ajili ya Kuchambua na Kushauri Kuhusu Ajira ya Majaji Baada ya Kustaafu’ chini ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Kikundi Kazi kiliwasilisha Taarifa yake Machi 7, 2008. Katika Taarifa yake Kikundi Kazi kinakubaliana na msimamo wa kikatiba kwamba “kwa kuzingatia Ibara za 110 na 120 za Katiba inaonekana wazi kuwa suala la ajira za mikataba kwa Majaji ambao wamekuwa wakifanya kazi za Jaji baada ya kufikia umri wa kustaafu ni kinyume cha Katiba.” Kwa mujibu wa Taarifa hiyo, hadi mwezi Machi 2008, “... walikuwepo Majaji wawili ... wa Mahakama ya Rufani na Majaji tisa ... wa Mahakama Kuu, ambao wapo katika ajira za mkataba, na Jaji mmoja ... wa Mahakama Kuu aliyeongezewa muda wa ajira kwa mujibu wa masharti ya Katiba....”

Hii ina maana kwamba, kulikuwa na Majaji kumi na moja ambao walikuwa wanafanya kazi kinyume cha Katiba na – kwa maneno ya Jaji wa Rufaa Luanda – hawakuwa Majaji kwa mujibu wa Katiba! Aidha, kwa mujibu wa ushahidi wa nyaraka hizi, kulikuwa na Jaji mmoja tu ambaye alikuwa ameongezewa muda wa ajira ya ujaji kwa mujibu wa Katiba. Katika mapendekezo yake, Kikundi Kazi hakikumung’unya maneno:

“Mikataba iliyopo hivi sasa iko kinyume cha Katiba.... Hii ina maana kwamba Majaji hao wanafanya kazi ya Jaji kinyume cha Katiba, hivyo kazi zote ambazo wamezifanya na wanaendelea kuzifanya wakiwa chini ya ajira mpya za mikataba hazina uhalali wowote kisheria. Kazi hizo ni sawa kama vile zimefanywa na mtumishi mwingine yeyote asiye na madaraka ya Jaji. Hivyo basi, Rais ashauriwe kuifuta mikataba hiyo mara moja kwa vile ina madhara makubwa kwa jamii na katika uteuzi wa Majaji wapya kuchukua nafasi zao. Majaji waliofutiwa mikataba waendelee na pensheni zao kama kawaida.”

Miaka minne imepita tangu Kikundi Kazi kiwasilishe mapendekezo yake Ikulu lakini hakuna hatua zilizochukuliwa kutekeleza mapendekezo hayo. Aidha, licha ya msimamo wa majaji Luanda na Ramadhani kuwa na umri wa takriban miaka saba, utaratibu wa uteuzi wa majaji wastaafu haujaachwa na mamlaka husika ya uteuzi. Ajira ya sasa ya Jaji Kiongozi Fakih Jundu iko katika kundi hili la watu wasiokuwa Majaji kwa mujibu wa Katiba.

JAJI KIONGOZI FAKIH JUNDU

Jaji Kiongozi Fakih Jundu aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu na Rais Mkapa mwaka 2003. Julai 29, 2009, Jaji Jundu wakati huo akiwa Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Iringa, alitoa taarifa ya kustaafu kwa mujibu wa sheria. Hata hivyo, mara baada ya kutoa taarifa hiyo, Jaji Jundu siyo tu alipewa mkataba wa ujaji kwa miaka mitatu, bali pia alipandishwa cheo na kufanywa Jaji Kiongozi.

Kama hiyo haitoshi, inasemekana sasa kwamba Jaji Kiongozi Jundu ameongezewa mkataba mwingine tena wa miaka miwili kuendelea kuwa Jaji Kiongozi kuanzia Julai 29, 2012! Huu ni ukiukaji wa Katiba. Kwanza, kwa mujibu wa Taarifa ya Kikundi Kazi, “... umri wa kustaafu wa Jaji Kiongozi ni miaka sitini.... Hivyo, iwapo Rais atamuongezea Jaji Kiongozi muda wa kufanya kazi, hatamuongezea kama Jaji Kiongozi.”

Kwa maana nyingine, kama ilikuwa makosa kikatiba kumpa Jaji Jundu mkataba wa ajira kama Jaji wa kawaida, ilikuwa makosa makubwa zaidi kikatiba kumpandisha cheo na kumfanya Jaji Kiongozi wakati alikwishafikisha umri wa kustaafu wa Jaji Kiongozi! Pili, kwa utamaduni uliozoeleka Tanzania, majaji wamekuwa wanaongezewa kipindi kimoja cha miaka miwili ili wamalizie kesi walizokuwa nazo hadi muda wao wa kustaafu unawadia. Kwa msimamo wa kikatiba ulioelezwa na Jaji wa Rufaa Luanda, Jaji Mkuu Ramadhani na Kikundi Kazi, siyo sahihi kwa Jaji Kiongozi Jundu kustaafu na kupewa mkataba wa kuendelea na wadhifa huo kupindukia muda wake wa kustaafu kwa mujibu wa Katiba!

Nyongeza hii ya pili ya mkataba wa Jaji Kiongozi Jundu imewafanya watu wanaojiita ‘Watumishi wa Mhimili wa Mahakama’ kumwandikia Msajili wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania kulalamikia jambo hilo. Kwa mujibu wa barua yao, ambayo pia ilinakiliwa kwa Mwanasheria Mkuu na Jaji Mkuu, watu hao wamesema yafuatayo kuhusu Jaji Kiongozi Jundu: “Sisi watumishi wa Mahakama tunafahamu udhaifu mkubwa kiutendaji alionao Jaji Kiongozi wetu wa sasa. Kimsingi hamudu madaraka haya. Ipo mifano mingi ya udhaifu wa Jaji Jundu. Mfano alimhamisha hakimu kutoka kituo chake cha kazi kama adhabu kwa vile hakimu huyo alitoa maamuzi ambayo yeye hakuyafurahiya kwenye ile kesi maarufu ya kibaragashia. Ni busara za Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman, ndizo zilizomsaidia hakimu huyo.”

JAJI THOMAS MIHAYO

Thomas Bashite Mihayo aliteuliwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Oktoba 8, 2003. Januari 16, 2006 Jaji Mihayo alitoa notisi ya kustaafu kwa mujibu wa Katiba kuanzia Juni 8, 2006 atakapokuwa ametimiza umri wa miaka sitini. Hata hivyo, Machi 8 ya mwaka huo, Jaji Mihayo alitaarifiwa na Jaji Mkuu kwamba Rais Kikwete alikuwa amempa “... mkataba wa miaka miwili kuanzia Juni 9, 2006.” Mkataba huo ulifikia mwisho wake Juni 8, 2008. Hata hivyo, Jaji Mihayo alipatiwa mkataba mwingine tena wa mwaka mmoja ulioanzia Juni 9, 2008 hadi Juni 8, 2009 na baada ya hapo hakupatiwa mkataba mwingine.

Inaelekea Jaji Mkuu Ramadhani alisahau msimamo wake wa awali kuhusu ajira za mikataba kwani ndiye aliyependekeza Jaji Mihayo “... apewe mkataba mwingine wa mwaka mmoja...” Na wala si Jaji Mihayo pekee aliyepatiwa au kuongozewa mkataba katika mazingira tatanishi kama haya. Kwa mujibu wa nyaraka za Idara Kuu ya Utumishi, Jaji Donasian Mwita alipatiwa mkataba wa ujaji Juni 28, 2004. Mkataba huo wa miaka miwili ulianza kutumika Julai 1, 2004. Vile vile, Jaji Joseph Masanche alisaini mkataba wa aina hiyo hiyo na Idara Kuu ya Utumishi ulioanza kutumika kuanzia Machi 7, 2006.

MAADILI YENYE SHAKA

Msemaji wa Kambi hakuzungumzia masuala yanayohusu maadili ya majaji. Hata hivyo, kutokana na mjadala uliojitokeza ndani na nje ya Bunge kutokana na hotuba yake, ushahidi umepatikana unaoonyesha kwamba baadhi ya majaji wameteuliwa bila ya kwanza kuwafanyia uchunguzi juu ya maadili yao.

MAJAJI KASSIM NYANGARIKA NA ZAINAB G. MURUKE

Kassim Nyangarika alikuwa wakili wa kujitegemea na wakili mwenza wa Jaji Kiongozi Jundu kabla ya uteuzi wake kuwa Jaji wa Mahakama Kuu mwaka 2003. Kama wakili, Bwana Nyangarika aliwahi kumwakilisha mlalamikaji katika kesi ya Peter Muti dhidi ya CIELMAC Ltd., Kesi ya Madai Na. 314 ya 2003 iliyofunguliwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni. Katika kesi hiyo mteja wa wakili Nyangarika alishinda.

Hata hivyo, kufuatia rufaa dhidi ya uamuzi huo, Mahakama Kuu ilifutilia mbali mwenendo wa kesi hiyo baada ya kugundua kwamba Wakili Nyangarika alikuwa amefanya vitendo vyenye kuashiria uvunjifu mkubwa wa maadili. Kwa mfano, Mahakama Kuu iligundua kuwa Wakili Nyangarika alimwelekeza hakimu – kwa kutumia ‘kipande cha karatasi cha rafu na kilichoandikwa kirafiki’ - namna ya kuendesha kesi hiyo. Mahakama Kuu iligundua makosa makubwa zaidi ya hilo. Kwa mujibu wa Jaji Kalegeya, “... kulikuwa na mawasiliano yasiyokuwa rasmi kati ya Mahakama na Wakili.” Jaji Kalegeya alikuta ushahidi wa uwezekano mkubwa kwamba Wakili Nyangarika ndiye aliyeandaa uamuzi wa Mahakama katika kesi hiyo. Aidha, Mahakama Kuu iligundua kwamba Wakili Nyangarika “... aliielekeza Mahakama kutokutoa uamuzi kwa tarehe iliyopangwa badala yake aliielekeza itoe uamuzi huo tarehe nyingine.”

Kwa mujibu wa Jaji Kalegeya, kama kilichoonyeshwa katika mawasiliano ya Wakili Nyangarika na Mahakama ya Wilaya kilikuwa cha kweli basi “... utoaji haki katika Mahakama hiyo uko katika hatari kubwa kama sio jina la Mahakama yote, kitu kinachohitaji marekebisho ya haraka.” Kwa sababu hiyo, Jaji Kalegeya alielekeza kwamba “mamlaka husika zichukue hatua za kufichua ukweli kuhusu barua ya Wakili Nyangarika ya tarehe 18/03/2004.” Hukumu na maelekezo ya Jaji Kalegeya yalitolewa tarehe 22 Julai, 2005. Miezi saba baadaye, Wakili Nyangarika aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania!

Wakili mwingine mwenye maadili ya mashaka yanayofanana na ya Jaji Nyangarika ambaye pia ameteuliwa Jaji Mahakama Kuu ni Zainab Muruke. Kama wakili, Zainab Muruke alimwakilisha Stephen Hill Forwood ambaye alikuwa amepatikana na hatia na kuhukumiwa adhabu ya kifungo cha miaka miwili bila faini katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu. Baadaye kampuni ya mawakili ya Z.G. Muruke & Co. Advocates iliwasilisha Hati ya Mapitio (Memorandum of Review) katika Mahakama hiyo hiyo ikiomba Bwana Forwood abadilishiwe hukumu.

Ombi hilo lilikubaliwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi Kabuta na tarehe 26 Julai, 2004, Bwana Forwood akabadilishiwa adhabu kuwa faini ya shilingi 20,000 au kifungo cha miaka miwili. Jambo hili liliripotiwa kwa Jaji Kiongozi ambaye aliamuru uchunguzi ufanywe uliopelekea kushushwa cheo cha Hakimu Mkazi Kabuta. Jaji Kiongozi pia aliamuru Wakili Muruke atoe maelekezo ya ushiriki wake katika sakata hilo. Hiyo ilikuwa tarehe 14 Desemba, 2004. Mwaka mmoja na miezi miwili baadaye, Zainab Muruke aliteuliwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

MAJAJI PELAGIA B. KHADAY NA PATRICIA FIKIRINI

Bi. Pelagia B. Khaday ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania aliyeteuliwa mwaka 2009. Kabla ya uteuzi huo Bi. Khaday alikuwa Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kabla ya hapo alikuwa Hakimu Mkazi Mkuu na Msajili wa Wilaya, Mahakama Kuu Kanda ya Arusha. Agosti 12, 2004, alipewa taarifa ya kusimamishwa kazi kama Msajili wa Wilaya na kuhamishiwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutokana na ‘uzito wa shutuma’ zilizotolewa dhidi yake kwa Jaji Mkuu.

Taarifa hiyo iliandikwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Edward Rutakangwa, kwa maelekezo ya Jaji Mkuu na ilieleza kwamba Bi. Khaday alikuwa anatuhumiwa kwa “kuwashinikiza au kuwashawishi baadhi ya mahakimu mkoani Arusha kushughulikia au kuamua kwa upendeleo mashauri yaliyowahusu ... jamaa au rafiki zake”; na “kuwaandalia sababu za rufaa baadhi ya washitakiwa waliotiwa hatiani na mahakama za mahakimu hapa mkoani.”

Kabla ya kumsimamisha Bi. Khaday kazi, Jaji Mfawidhi Rutakangwa alikuwa amemteua Mheshimiwa Jacob Somi, wakati huo akiwa Msajili wa Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi, kuwa Afisa Uchunguzi (Enquiry Officer) ili kuchunguza tuhuma dhidi ya Bi. Khaday. Taarifa ya Uchunguzi wa Awali ya Afisa Uchunguzi Somi inasema kwamba Bi. Khaday alikuwa amelalamikiwa na mahakimu kwa kuwashinikiza ili watoe maamuzi ya kesi zilizokuwa zinawakabili jamaa au marafiki zake.

Kwa mujibu wa Taarifa hiyo, Hakimu Mkazi Elvin Mugeta “alikiri kuwa-approached na Bi. Khaday ili atoe hukumu ya upendeleo kwa mshtakiwa Richard Bareto ambaye inasadikiwa kuwa ni jamaa wa rafiki yake wa karibu.” Ijapokuwa Bi. Khaday alikanusha kufanya hivyo, Afisa wa Uchunguzi Somi aliridhika kwamba “Bi. Khaday alikuwa amejiwekea utaratibu, kama alivyodai mwenyewe, wa kuwasiliana na Mahakimu kwa lengo la kuwafahamisha pamoja na mambo mengine malalamiko yaliyokuwa yakimfikia dhidi yao ili kuwanusuru wasiharibikiwe.”

Hata hivyo, Afisa Uchunguzi Somi aliridhika kwamba “utaratibu huu ulikuwa kero kwa mahakimu pale alipoutumia kwa kushinikizwa na jamaa zake na/au rafiki zake kwa lengo la kupata maamuzi ya upendeleo. Kitendo cha kumtoa mahakamani Hakimu kwa lengo la kutaka kujua hatima ya mshtakiwa Bareto aliyekuwa asomewe hukumu siku hiyo, ni mfano wa matumizi mabaya ya utaratibu huo.”

Afisa Uchunguzi Somi hakupata uthibitisho wa madai ya Bi. Khaday kuwaandalia sababu za rufaa washtakiwa waliotiwa hatiani. Hata hivyo, kwa mujibu wa Taarifa yake, “... sikuridhishwa na utaratibu wake wa kupeleka nakala ya hukumu kwa Bi. Mushi na kumtaka aisome ili kuona kama kuna uwezekano wa mshtakiwa Hussein Ramadhani Kitema kukata rufaa Mahakama Kuu baada ya kufungwa jela na Bw. Mugeta.” Afisa Uchunguzi Somi alipendekeza kwamba Bi. Khaday – “ambaye ni mtumishi wa Mahakama kwa kipindi kisichopungua miaka 20...” - apewe nafasi ya kujirekebisha.

Baada ya kuwasilishwa kwa Taarifa ya Afisa Uchunguzi Somi, Jaji Mfawidhi Rutakangwa alimteua Mh. Samuel Karua, Msajili wa Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi, kuwa Investigation Officer. Tarehe 23 Februari 2007, Investigation Officer Karua aliwasilisha Taarifa ya Uchunguzi wake kwa Jaji Mkuu. Taarifa ya Investigation Officer Karua ilimkosha Bi. Khaday kwa tuhuma zote dhidi yake.

Hata hivyo, Taarifa ya Investigation Officer Karua ina maeneo mengi yanayoleta mashaka. Kwanza, kama Investigation Officer Karua mwenyewe alivyosema, shahidi muhimu katika uchunguzi wake alikuwa Hakimu Mkazi Mfawidhi Mushi. Vile vile, shahidi huyu alikuwa ‘star witness’ katika uchunguzi wa awali mbele ya Afisa Uchunguzi Somi na ndiye aliyetoa ushahidi wa yeye na mahakimu wengine kuingiliwa katika kazi zao na Bi. Khaday.

Hata hivyo, mbele ya Investigation Officer Karua, shahidi huyu muhimu alikana kila kitu alichokisema mbele ya Afisa Uchunguzi Somi. Kwa kiasi kikubwa, Investigation Officer Karua aliitumia about turn hii kumkosha Bi. Khaday dhidi ya tuhuma zote zilizokuwa zinamkabili. Cha kushangaza ni kwamba Investigation Officer Karua hakujiuliza na hakumuuliza shahidi huyu sababu za kukana ushahidi wote alioutoa mbele ya Afisa Uchunguzi Somi.

Je, alirubuniwa au kutishwa ili amsaidie Hakimu na mtumishi mwenzake katika Mahakama ya Tanzania asifukuzwe kazi? Kama sio hivyo, je, ni sababu zipi zilizomfanya shahidi huyu muhimu kubadili ushahidi wake kwa kiasi hicho? Je, ushahidi alioutoa shahidi huyu mbele ya Afisa Uchunguzi Somi ulikuwa wa uongo? Na kama ulikuwa wa uongo, ushahidi wake wa pili kwa Investigation Officer Karua ni wa kweli kiasi gani mpaka kumfanya Investigation Officer Karua kutamka kuwa shahidi huyu ‘anaweza ... kuwa anasema ukweli.’

Inaelekea Investigation Officer Karua, Hakimu Mkuu Mkazi mwenye uzoefu wa miaka mingi katika Mahakama, alifanya kazi yake kwa mtazamo wa kimahakama zaidi badala ya kutumia mtazamo wa kiupelelezi na/au kiuchunguzi ambayo hasa ndiyo ilikuwa kazi yake katika uchunguzi wa tuhuma dhidi ya Bi. Khaday. Kwa mtazamo wa kimahakama, ukweli kwamba shahidi muhimu kama Hakimu Mkazi Mfawidhi Mushi alikana ushahidi wake wa awali mbele ya Afisa Uchunguzi Somi ilikuwa inatosha kumfutia Bi. Khaday hatia yote. Kwa mtazamo wa kiupelelezi/kiuchunguzi, about turn ya shahidi huyu ingemfanya Investigation Officer Karua kuchunguza zaidi sababu za kigeugeu hicho.

Pili, Investigation Officer Karua hakuipa uzito wa kutosha Taarifa ya Afisa Uchunguzi Somi. Kwa mfano, Taarifa ya Afisa Uchunguzi Somi – yenye kurasa 14 zilizochapwa - imeelezewa katika Taarifa ya Investigation Officer Karua kwa aya moja tu! Kwa sababu hiyo, ni vigumu kukubaliana na Investigation Officer Karua kwamba Taarifa ya Afisa Uchunguzi Somi ‘ilikuwa muhimu sana’ wakati umuhimu huo haujafafanuliwa wala kuelezewa hata kidogo katika Taarifa yake.

Aidha, Investigation Officer Karua alitakiwa kueleza sababu za kutofautiana na Afisa Uchunguzi Somi kwamba Bi. Khaday alikuwa anakera mahakimu kwa kuwasiliana nao baada ya kushinikizwa na ndugu au rafiki zake ili wapatiwe upendeleo katika kesi zilizokuwa zinawakabili. Investigation Officer Karua hakufanya hivyo. Vile vile, Investigation Officer Karua hakuona ajabu wala kujiuliza kama ilikuwa ni kitu cha kawaida kwa Bi. Khaday kumleta Richard Bareto – mshtakiwa aliyehusishwa na shinikizo la Bi. Khaday kwa Hakimu Mkazi Mugeta – kama shahidi wake wa utetezi.

Tatu, Investigation Officer Karua hakutoa sababu za maana za kutochukua ushahidi wa mahakimu wengine waliodaiwa kushinikizwa na Bi. Khaday. Katika aya moja tu iliyowahusu mahakimu hao, Investigation Officer Karua alisema kwamba siku ya kutoa ushahidi wao kwake, watu hao “... walishikilia msimamo wa kauli walizotoa mbele ya Bwana Somi ... na baada ya tafakuri ya muda ... mashahidi hawa waliachiwa.”

Mbele ya Afisa Uchunguzi Somi, mashahidi hawa wawili, Hakimu Mkazi Msumi na Hakimu Mkuu wa Wilaya Mlay, walikuwa wamesema kwamba “... huko nyuma (Bwana Msumi) aliwahi kuitwa na mlalamikiwa baada ya wadhamini walioshindwa kukidhi masharti ya dhamana ... kumpelekea malalamiko ya kukataliwa dhamana, maelezo ambayo hayakuwa na ukweli wowote.” Aidha, kwa mujibu wa Afisa Uchunguzi Somi, “... katika hali isiyokuwa ya kawaida Bw. Mlay, PDM hakuwa tayari kueleza kilichomsibu hadi kujiengua katika usikilizaji wa kesi ambayo Bi. Mushi alidai ilikuwa inamkabili rafiki yake wa karibu na Bi. Khaday.” Investigation Officer Karua hakuona sababu yoyote ya kufuatilia ushahidi wa mahakimu hawa wawili!

Nne, Investigation Officer Karua anakubali kwamba hali ilikuwa tete katika Kituo cha Arusha: “Inaelekea mtuhumiwa alikuwa na mahusiano mabaya na baadhi ya mahakimu.” Kama hivyo ndivyo ilivyokuwa, Investigation Officer Karua alikuwa na wajibu wa kuchunguza chanzo cha mahusiano hayo mabaya, hasa kwa vile kulikuwa sio tu na tuhuma bali pia ushahidi wa mahakimu husika kwamba Bi. Khaday alikuwa anawaingilia mahakimu katika kazi zao. Hakufanya hivyo. Badala yake Taarifa ya Investigation Officer Karua inaonekana kama jitihada za kumkosha Bi. Khaday dhidi ya tuhuma nzito za ukosefu wa maadili ya kimahakama. Jitihada hizi zilifanikiwa kwani miaka miwili baada ya Taarifa ya Investigation Officer Karua, Bi. Khaday aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Na wala siyo Bi. Khaday pekee aliyeneemeka na taarifa hiyo. Bi. Patricia Fikirini, ambaye Taarifa ya Afisa Uchunguzi Somi inamwelezea kama mmoja wa mahakimu waliosikiliza kesi ya mfanyabiashara maarufu wa Arusha, Justin Nyari iliyokuwa chanzo cha tuhuma dhidi ya Bi. Khaday – alihusishwa na tuhuma dhidi ya Bi. Khaday kwa maneno yafuatayo: “... Kama mtawala ... (Bi. Khaday) ... alisema aliwahi, tena kwa nia njema, kumweleza Bi. Fikirini ... kuhusu uvumi kwamba mume wake alikwenda gerezani na kuchukua mamilioni ya fedha kwa Bw. Nyari na hivyo kumshauri awe mwangalifu zaidi”! Katika uteuzi wa majaji uliofanywa na Rais Kikwete mwezi Juni mwaka huu, Bi. Patricia Fikirini naye ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Wapo wanaoweza kusema kwamba Bi. Khaday hakupatikana na hatia yoyote na kwa hiyo haikuwa makosa kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu. Aidha, inaweza kudaiwa kwamba Bi. Fikirini hajawahi kutuhumiwa kwa kosa lolote la maadili na kwamba ‘uvumi’ pekee hautoshi kumnyima mtu mwenye sifa haki ya kuteuliwa Jaji wa Mahakama Kuu. Kwa wenye hoja za aina hii jibu langu ni kwamba kiwango cha ‘sifa maalum’ kinachotakiwa na Katiba kwa mtu kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ni mtu ambaye “... kwa kila hali anafaa kukabidhiwa madaraka ya Jaji wa Mahakama Kuu....” Kiwango hiki ni cha juu kiasi kwamba kutokuwa na hatia pekee haitoshi kumfanya mhusika kuwa ‘kwa kila hali anafaa kukabidhiwa madaraka ya Jaji wa Mahakama Kuu.’ Kwa maoni yangu, mtu aliyeundiwa uchunguzi wa kimaadili au ambaye kuna uvumi unaomhusisha na rushwa ‘hafai kwa kila hali’ kukabidhiwa madaraka ya Jaji wa Mahakama Kuu. Majaji Khaday na Fikirini wapo kwenye kundi hili.

JAJI ALOYSIUS MUJULIZI

Jaji Aloysius Mujulizi alikuwa miongoni mwa watu ishirini walioteuliwa Majaji wa Mahakama Kuu mwezi Februari, 2006. Kabla ya uteuzi wake, Jaji Mujulizi alikuwa wakili wa kujitegemea katika kampuni ya mawakili ya Ishengoma, Masha, Magai & Mujulizi Advocates (IMMMA) ya Dar es Salaam. Kampuni hii ya mawakili ndiyo iliyoshiriki katika kuanzishwa kwa kampuni iitwayo Deep Green Finance Co. Ltd. mnamo tarehe 18 Machi 2004. IMMMA Advocates vile vile walikuwa mawakili wa Tangold Ltd.

Makampuni haya mawili yanatuhumiwa kutumika kupitishia mabilioni ya fedha zilizoibiwa Benki Kuu ya Tanzania kati ya mwaka 2005 na 2006. Kwa mfano, katika kipindi kifupi cha miezi minne kati ya Agosti 1 na Desemba 10, 2005 kampuni ya Deep Green Finance ilipokea jumla ya shilingi 10,484,005,815.39 kutoka akaunti ya kulipia madeni ya nje (EPA) iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania. Katika kipindi hicho hicho, kampuni ya Tangold Ltd. ililipwa dola za Marekani 13,736,628.73 kutoka kwenye akaunti hiyo ya EPA. Nyaraka zilizowasilishwa BRELA na mawakili wa IMMMA Advocates na kusainiwa na Gavana wa Benki Kuu wa wakati huo Daudi Ballali tarehe 20 Mei 2005 zinaonyesha kwamba Tangold Limited ilikuwa kampuni ya kigeni kutoka Jamhuri ya Mauritius. Haya yote yalitokea wakati Jaji Mujulizi akiwa wakili mwenza wa IMMMA Advocates.

‘SIFA MAALUM’ ZENYE SHAKA

JAJI WA RUFAA MBAROUK SALIM MBAROUK

Mbarouk Salim Mbarouk aliteuliwa kuwa Jaji wa Rufaa wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania mwaka 2008. Kabla ya uteuzi huo Jaji Mbarouk alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar. Sifa za mtu kuteuliwa kuwa Jaji wa Rufaa zimeainishwa katika ibara ya 118(3) ya Katiba: “Majaji ... wa Rufani watateuliwa na Rais, kwa kushauriana na Jaji Mkuu, kutoka miongoni mwa watu wenye sifa za kuteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ... zilizoainishwa katika Ibara ya 109 ya Katiba au kutoka miongoni mwa watu wanaoweza kuteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar kwa mujibu wa sheria zinazotumika Zanzibar na wamekuwa na sifa hizo kwa muda usiopungua miaka kumi na tano.”

Kwa mujibu wa Ibara ya 94(3) ya Katiba ya Zanzibar, 1984, “mtu hatoweza kuteuliwa kuwa Jaji au Kaimu Jaji wa Mahkama Kuu mpaka awe na shahada ya Sheria ya Chuo Kikuu kinachotambuliwa au Chuo cha aina hiyo; au awe au amewahi kuwa Jaji wa Mahkama zilizofanana na hii kwa kesi zote za jinai na madai katika Tanzania au sehemu yoyote ya Jumuiya ya Madola au Mahkama ya Rufaa kutoka Mahkama hizo; au awe Mwanasheria wa Zanzibar au Tanzania kwa kipindi kisichopungua miaka saba; au awe na uzoefu wa Jaji au mwanasheria kwa pamoja usiopungua miaka saba.” Jaji Mbarouk hajatimiza hata moja ya masharti hayo ya Katiba ya Zanzibar. Jaji huyu hana shahada yoyote ya sheria inayotambuliwa na mamlaka ya ithibati ya Tanzania kama inavyotakiwa na Ibara ya 109(7) ya Katiba. Jaji huyu ana stashahada ya juu ya sheria (Post Graduate Diploma in Law) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Shahada ya Uzamili ya Sanaa ya Chuo Kikuu cha nchini Uingereza.

Uteuzi wa Jaji Mbarouk kuwa Jaji wa Rufaa ulileta minong’ono mingi katika taaluma ya sheria kiasi kwamba marehemu Wakili Leopold Kalunga anasemekana kufungua shauri katika Mahakama Kuu ya Tanzania kutaka uteuzi huo utenguliwe. Hata hivyo, Wakili Kalunga alifariki kabla ya shauri lake kusikilizwa na kwa hiyo liliondolewa mahakamani. Aidha, monong’ono hiyo ilimfanya Jaji wa Rufaa Mbarouk kujiunga na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ambako bado ni mwanafunzi hadi ninapoandika Addendum hii.

MAJAJI ‘WALIOTOLEWA MITAANI’

Katika Maoni ya Kambi tulidai kwamba “... sasa watu wanateuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ambao hawajawahi kupendekezwa na Tume ya Utumishi wa Mahakama na - kwa sababu hiyo - hawajafanyiwa vetting yoyote na mamlaka hiyo ya kikatiba....” Ukiacha uteuzi wa Jaji wa Rufaa Mbarouk ambao haubanwi na masharti ya Ibara ya 109(1) na 113(1)(a) ya Katiba, majaji wengine waliotajwa kwenye Addendum hii hawakupendekezwa na Tume ya Utumishi wa Mahakama. Majaji wengine ambao pia hawajawahi kupendekezwa na Tume hiyo ni pamoja Fatuma Massengi, Mary Sumari, Imani Mkwawa-Aboud na Sekela Mushi.

 

Tuesday, August 14, 2012

Maalim Seif: Tunataka kiti cha Zanzibar UN kirudishwe

                                         
 Na Mwinyi Sadallah | 14th August 2012

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, amesema kuna haja kwa Zanzibar kurejeshewa kiti chake katika Umoja wa Mataifa (UN).


Alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na viongozi wa wilaya na majimbo wa Chama cha Wananchi (CUF) katika ukumbi wa Benjamin Mkapa, kisiwani Pemba jana.


Alisema Zanzibar kabla ya Muungano ilikuwa nchi huru iliyokuwa na kiti chake UN na kuelezea haja ya kuwepo kwa mamlaka kamili ya Zanzibar ili iweze kurejesha kiti chake kwenye umoja huo.


Maalim Seif alisema hoja kubwa ambayo Wazanzibari wanatakiwa kujadili katika mchakato wa maoni ya Katiba mpya ni muundo na mfumo wa Muungano.


“Zanzibar tunayo Katiba yetu ya mwaka 1984 ambayo imejitosheleza kwa mambo yetu ya Zanzibar, lakini suala kubwa kwenye mabadiliko hayo kwetu sisi litakuwa ni la Muungano na hili haliwezi kuepukwa,” alisema Maalim Seif.


Maalim Seif aliwataka wananchi kuangalia maslahi ya nchi yao kwanza katika mchakato wa kukusanya maoni ya mabadiliko ya katiba na kuacha tabia ya kutetea misimamo ya vyama badala ya maslahi ya nchi na wananchi wake.


“Katiba ya nchi ni mali ya wananchi siyo ya chama chochote, lakini najua kila chama kina katiba yake na hiyo ndiyo itabakia kuwa katiba na mwongozo wa chama husika, kwa hivyo ndugu zangu naomba tulifahamu hili na tuangalie maslahi ya nchi yetu kwanza,” alisema Maalim na kupigiwa makofi na wanachama.


“Mimi najua wapo wanaotaka serikali moja, wengine mbili, tatu, nne, na muungano wa mkataba, lakini wengine wanataka waachiwe wapumue…Yote hayo ni maoni na kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake bila ya kulazimishwa, kwa hivyo wakati wenu ukifika nendeni mkatoe maoni hayo kwa uwazi,” alisema Maalim Seif.


“Wakati wenu ukifika nendeni mkatoe maoni yenu kwa uwazi bila ya hofu hiyo ni haki yenu ya kikatiba,” aliongeza.
Alisema serikali ya Tanzania tayari imepanga ifikapo Aprili 2014, Tanzania iwe na katiba mpya ambayo inatokana na matakwa ya wananchi wake wa pande mbili za Muungano huo.


Ingawa Maalim Seif hakufafanua kauli yake ya Zanzibar kuwa na kiti chake katika UN, lakini anamaanisha kwamba Zanzibar inapaswa kuwa na mamlaka yake kamili.


Kwa maana hiyo ikiwa Zanzibar itarejeshewa kiti chake katika UN hapatakuwepo na Muungano tena kwa kuwa itakuwa ni nchi kamili ambayo inatambuliwa na UN na jumuiya ya kimataifa kwa ujumla.

Tangu Tume ya kukusanya maoni ya Katiba mpya kuanza kazi hiyo, kumeibuka kikundi kinachofanya kampeni misikitini (Uamsho) kutaka Zanzibar kujitenga katika Muungano huku wengine wakitetea kuwepo kwa Muungano wa mkataba.

Vile vile, baadhi ya Wazanzibari wakiwemo mawaziri na makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamesema kuwa kuna haja ya kuwa na Muungano wa mkataba kwa lengo la kumaliza kero zinazolalamikiwa.

Baadhi ya makada wa CCM waliotaka Muungano wa mkataba ni Waziri asiye na Wizara Maalum, Mansour Yusuf Himid na mmoja wa waasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar, Ali Nassoro Moyo.
Hata hivyo, baadhi ya makada wamewashambulia na kuwatisha wanachama wa chama hicho wanaotoa maoni tofauti na sera ya CCM ambayo ni muundo na mfumo wa serikali mbili.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi, wiki iliyopita wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Jimbo lake la Kitope, alisema wanaopingana na sera ya CCM kuhusu muungano warejeshe kadi zao za uanachama badala ya kusubiri kufukuzwa.

Naye Mbunge wa Uzini (CCM), Dk. Mohammed Seif Khatib, Alhamisi iliyopita akizungumza na waaandishi wa habari mjini Dodoma akiwa na wabunge zaidi ya 30 kutoka Zanzibar alieleza kushangazwa na wanachama wanaotoa maoni ya kuvunja Muungano.

Khatib ambaye ni Mwenyekiti wa wabunge wa CCM Zanzibar, alisema chama hicho kinapaswa kuwachukulia hatua kwa maelezo kuwa walipata nyadhifa zao kwa kutumia ilani ya CCM inayoeleza wazi kuwa sera yake ni ya Muungano wa serikali mbili.

CHANZO: NIPASHE

Monday, August 13, 2012

Dk Ulimboka: Niko tayari kwa lolote


ALAKIWA DAR KWA KISHINDO, ASEMA NIKO FITI TAYARI KWA KAZI

Raymond Kaminyoge na Geofrey Nyang’oro

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Stephen Ulimboka amerejea nchini jana akitokea Afrika Kusini alikokuwa akitibiwa na kulakiwa na mamia ya watu huku akisema haogopi lolote na yupo tayari kwa kazi.
Dk Ulimboka aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere saa 8.15 mchana kwa ndege ya Shirika la South African Airways.
Baada ya kumaliza taratibu zote uwanjani na kutoka nje, Dk Ulimboka alilakiwa na umati mkubwa wa wananchi wakiwemo madaktari na wanaharakati ambao walijaza karibu eneo kubwa la lango la abiria wanaowasili jambo lililoonekana dhahiri kumsisimua kiasi hadi kufikia kububujikwa wa machozi.
Dk Ulimboka ambaye alipelekwa Afrika Kusini akiwa hawezi kutembea wala kula mwenyewe baada ya Juni 27 mwaka huu kutekwa na watu wasiojulikana, kupigwa na kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili, kisha kutupwa katika Msitu wa Pande, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, amerejea akiwa anatembea na mwenye afya njema.
Akizungumza uwanjani hapo, Dk Ulimboka alisema: “Nawashukuru Watanzania kwa kuniombea, nawashukuru madaktari wenzangu, ndugu na jamaa zangu kwa kunisaidia kupata matibabu hadi leo hii narudi nyumbani nikitembea mwenyewe. Hivi sasa niko fiti na niko tayari kwa kazi yoyote.”
Uwanja huo ulikuwa umefurika mamia ya wananchi wakiwemo madaktari ambao walikuwa na shauku ya kumwona Dk Ulimboka, lakini wengi hawakufanikiwa kumwona.
Wingi wa watu ulisababisha kutokea kwa msuguano kati ya madaktari na waandishi wa habari. Wakati wanahabari wakitaka kumwuliza maswali Dk Ulimboka, baadhi ya madaktari walikuwa wakimzuia Dk Ulimboka kujibu maswali licha ya mwenyewe kuonekana kuwa tayari kuulizwa.
Baadhi yao walifikia hatua ya kushika kamera za waandishi huku wengine wakisema... “Mwacheni akapumzike bwana, kwa nini mnamsumbua sumbua.”
Baadhi ya madaktari hao walifikia hatua ya kutumia nguvu dhidi ya wapiga picha wa magazeti na televisheni na hivyo kusababisha vurugu na kelele nyingi katika eneo hilo.
Muda wote wakati Dk Ulimboka akielekea kwenye gari akiwa na maua mkononi aliyokadhibiwa baada ya kuwasili uwanjani hapo, madaktari hao walikuwa wakiimba nyimbo za kuhamasishana ukiwamo Wimbo wa Taifa huku wengine wakisema: “Mtakufa nyie, lakini si Dk Ulimboka.”
Baada ya kupanda gari aina ya Nissan Patrol nyeusi, madaktari hao na wanaharakati na wananchi wengine wakiongozwa, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa), Ananileya Nkya walilisukuma gari hilo hadi katika lango la kutokea katika uwanja huo.

Wanaharakati
Mbali na Nkya, kulikuwa na idadi kubwa ya wanaharakati wengine wakiongozwa na Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP, Usu Malya.
Wanaharakati hao walikuwa na mabango yaliyoandikwa, “Dk Ulimboka karibu nyumbani uliumizwa kikatili ukitetea afya bora kwa Watanzania.”
Bango jingine lilisomeka: “Dk Ulimboka damu yako ilimwagika na kuamsha ari kwa wananchi kudai za afya.”
Jingine, “Dk Ulimboka wewe ni mpigania haki ya afya bora kwa wananchi wote Mungu na Watanzania wote tuko nawe.”
Malya akizungumza uwanjani hapo alisema kupona kwa Dk Ulimboka na kurejea nchini ni uthibitisho kwamba Mungu amesikia sauti za wanyonge.
“Dk Ulimboka alisimamia haki za madaktari na za Watanzania wote akitaka huduma bora zipatikane kwenye hospitali za umma kwa ajili ya Watanzania wote,” alisema.
Mkurugenzi wa Tamwa, Nkya alisema amefurahi kumpokea Dk Ulimboka akiwa hai kwa sababu hali yake ilikuwa mbaya wakati akipelekwa kwa matibabu nje ya nchi.
Kwa upande wake, Katibu wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Edwin Chitage alisema kurejea kwa Dk Ulimboka akiwa amepona kunathibitisha kwamba nchi za wenzetu kuna vifaa vya tiba za kisasa na dawa.
“Kurejea kwa Dk Ulimboka ni mapenzi ya Mungu, huu ni uthibitisho kuwa hapa nchini hakuna vifaa tiba na dawa zinazoweza kusaidia wananchi kama ilivyo kwa wenzetu,” alisema Dk Chitage na kuongeza:
“Madaktari tumefarijika na hii imetupa nguvu licha ya vitisho tunavyopata tutaendelea kupigania haki zetu, haya ni mapambano ya muda mrefu, ”alisema.
Dk Chitage alisema kupona na kurejea nchini kwa Dk Ulimboka ni uthibitisho kuwa watu wengi wasio na uwezo wanapoteza maisha kutokana na kukosekana kwa vifaa tiba na dawa hapa nchini... “Madaktari tupo, lakini tatizo ni vifaa na dawa, hiki ndicho tunachopigania ni haki wananchi kupata huduma za afya nchini.”
Katibu Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk Rodrick Kabangila alisema kurejea kwa Dk Ulimboka kutasaidia kuwatambua watu waliohusika katika tukio la kumteka, kumpiga na kumtupa katika Msitu wa Pande.
“Sisi tumefurahi sana, Dk Ulimboka alisimamia haki za madaktari na sekta ya afya kwa ujumla, kurudi kwake kunatupa nguvu ya kuendelea kudai haki za madaktari na wananchi,” alisema.
Dk Ulimboka anarejea nchini huku Serikali na madaktari wakiwa hawajafikia mwafaka kuhusu madai yao.
Madai ya madaktari hao ni hali bora ya mazingira ya utoaji afya nchini, ongezeko la mishahara, posho za kufanya kazi katika mazingira magumu, posho za kufanya kazi katika mazingira hatarishi na posho za kuitwa kazini.

Safari ya Dk Ulimboka kwenda kwenye matibabu nchini Afrika Kusini ilitawaliwa na usiri mkubwa alipoondoka nchini Juni 31 mwaka huu, akisindikizwa na Dk Pascal Lugajo na kaka yake, Dk Hobakile Ulimboka na mke wake, Dk Judith Mzovela.

Kutekwa
Dk Ulimboka alitekwa na kufanyiwa vitendi vya ukatili wakati akiratibu mgomo wa madaktari uliokuwa ukiendelea na aliokotwa na msamaria mwema akiwa amefungwa mikono na miguu akiwa katika hali mbaya.
Kutokana na tukio hilo, wanaharakati wa haki za binadamu waliituhumu Serikali kuhusika na tukio hilo, huku Serikali ikikana na kuliagiza Jeshi la Polisi kuwasaka waliohusika.
Akisimulia mkasa huo Dk Ulimboka alisema tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Juni 27 katika Klabu ya Leaders, Dar es Salaam alikokuwa na daktari mwenzake na mtu mwingine aliyekuwa amemwita hapo (Leaders).
“Mara, katikati ya maongezi tukaona huyo mtu aliyeniita anaongea na simu. Ghafla tukiwa tunasema tuagane, wakaja watu kama watano hivi na bunduki, wakasema wewe na yule bwana mko free (huru), tunakuchukua wewe (Dk. Ulimboka). Sijakaa sawa, nikaona nimeshaburutwa nikaanguka kwenye lami, wakaniinua na kuniingiza kwenye gari nyeusi, lakini ilikuwa haina namba.”
Wakati Dk Ulimboka alipokuwa akiendelea na matibabu Afrika Kusini, Rais Jakaya Kikwete alisema Serikali haihusiki na kilichomtokea daktari huyo kwa kuwa alikuwa kiungo muhimu katika majadiliano baina ya Serikali na madaktari.

Rais Kikwete alisema hayo katika hotuba yake ya mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.
“Dk Ulimboka alikuwa kiungo muhimu katika mazungumzo baina ya Serikali na madaktari. Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyo hakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya. Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo, lakini nilisema wamuache maadam madaktari wanamwamini kuwa anaweza kuwasemea vizuri zaidi kuliko wao wenyewe walioajiriwa na Serikali,” alisema Rais Kikwete.
Alisema alichofanyiwa Dk Ulimboka kimemsikitisha na kumhuzunisha kwa kuwa ni kitendo cha kinyama na kinyume kabisa na mila na desturi za Tanzania.
Kauli ya Rais Kikwete kuhusu mgomo wa madaktari inafanana na ile iliyokuwa imetolewa awali na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisema wanatambua kuwa Serikali nayo inatajwa katika orodha ya wanaotiliwa shaka kuhusu kilichomtokea Dk Ulimboka, lakini ameshangazwa na hisia hizo akisema haoni sababu ya Serikali kufanya hivyo.

Dk Ulimboka alisafirishwa kwenda Afrika Kusini Juni 31, mwaka huu kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi baada ya jopo la madaktari waliokuwa wakimhudumia, kueleza mabadiliko ya hali ya afya yake, yaliyosababisha figo kushindwa kufanya kazi.

Ulinzi nyumbani
Nyumbani kwao, eneo la Ubungo Kibangu kulikuwa na watu kadhaa waliokuwa nje ya nyumba huku ulinzi ukiwa umeimarishwa.
Vijana wasiopungua watatu wakiwa wamevaa kawaida walikuwa wamekaa jirani na lango la kuingilia wakiratibu nyendo za wanaopita na wanaotaka kuingia katika nyumba hiyo iliyopo karibu na Shule ya Msingi Ubungo Kibangu.
“Watu walikuwa wengi hapa lakini wametakiwa kuondoka ili kutoa nafasi kwa dokta kupumzika na hakuna ambaye anaruhusiwa kuingia kwa sasa labda kama ni daktari mwenzao,” alisema kijana mmoja anayeishi jirani.
Awali, mama mmoja ambaye alifahamika kama ndugu wa familia hiyo anayeishi karibu na nyumba ya Dk Ulimboka alipoulizwa nyumbani kwa kiongozi huyo wa madaktari alihoji anatafutwa na nani na hata mwandishi walipojitambulisha alimtaka aondoke na kurejea alikotoka.
“Baba wewe nenda nyumbani kwako tu, usitake kujua zaidi,” alisema mama huyo majibu ambayo yalionekana kufanana na ya majirani wengi wa daktari huyo.
Nyongeza na Joseph Zablon