Habari wanablog:
Hakika kwa yeyote anayetaka kuanzisha biashara yampasa kuwa makini na aina ya biashara anayotaka kuanzisha. Kumbuka lengo la kuanzisha biashara (mradi) ni kujipatia faida ama kuhakikisha mteja anaridhika na kile anachokipata. Kuna mambo ya msingi kadhaa ambayo mjasiriamali anaweza kutumia kama muongozo katika kuanzisha mradi mpya.
Uainishaji wa Fursa (opportunity identification)
Kabla hujaanzisha mradi jambo la muhimu na la msingi ni kuainisha fursa zilizopo katika eneo linalokuzunguka. Fursa ni mazingira chanya na saidizi ambayo mjasiriamali anatumia kuanzisha mradi na kujipatia faida nyingi kwa muda mfupi ama mrefu. Mara tu mjasiriamali anapotambua fursa zilizopo na kuamua kuanzisha mradi, akijua kuwa matarajio ya mradi huo ni chanya basi mjasiriamali huyo uwekezaji wake una matarajio yafuatayo.
- Mradi kuwa na mapato mazuri na endelevu
- Mradi kuwa na soko la uhakika
- Gharama za uendeshaji wa mradi kuwa nafuu
- Mradi kuwa na uwezekano wa kukua.
Utakapojiridhisha kuwa hayo ya juu yanaweza kudhihiri, basi unaweza kuwekeza na kuanzisha mradi wa bidhaa ama utoaji huduma, kwa sababu kuna uwezekano mkubwa wa upatikanaji wa faida.
Vyanzo vya utambuzi wa fursa
- Mabadiliko ya teknolojia- hapa tumeona jinsi makundi mbalimbali yalivyofaidika na mabadilikoya teknolojia..Mfano watu wamejiajiri kupitia huduma za simu na kujipatia faida kupitia M-pesa, Tigo-pesa, Airtel money.....zamani fursa hizi hazikuepo. Pia kuna blogs za kibiashara mbali mbali zimeanzishwa nia na lengo ni kujipatia kipato kupitia kwa wadhamini: Mfano Mjengwa blog, Michuzi blog na jamii forum. Bado hujachelewa fursa zinazopatikana juu ya mabadiliko ya teknolojia zipo nyingi na kwenye sekta tofauti tofauti.
- Uelewa- Kwenye jamii yoyote uelewa wa mambo unapoongezeka huambatana na fursa mbali mbali za kiuchumi zinazoendana na kuongezeka kwa uelewa. Mathani mahitaji ya vyakula vilivyo salama na kemikali umekuwa mkubwa, kulinganisha na vyakula vinavyotokana na kemikali, hii ina sababishwa na watu kuwa na elimu juu ya madhara ya kemikali mwilini.
- Mabadiliko ya sera-
Itaendelea: Niandikie mmlanzi@yahoo.com