Nilitaka kuandika makala ndefu lakini nimeona niende moja kwa moja na kusema ombi/pendekezo langu kama litampendeza Rais Kikwete.
KWA KUWA, matokeo ya kidato cha nne ambayo yametoka hivi karibuni yameonesha kufeli kwa kutisha kwa watoto wetu katika mtihani wao;
KWA KUWA, kufeli huko kuna matokeo ya moja kwa moja katika maisha ya wanafunzi hawa, familia zao na kwa taifa kwa u jumla;
KWA KUWA, matokeo hayo ni hasara kubwa kwa wazazi waliowekeza kwa miaka minne ya elimu ya watoto hawa na kwa taifa katika kuwekeza vifaa, walimu na miundo mbalimbali;
KWA KUWA, kuacha kundi kubwa la watoto hawa kurudi katika maisha ya uraiani kutaongeza jamii ya watu ambao hawana elimu ya kutosha na wasioweza kuajiriwa hata katika mifumo isiyo rasmi (pamoja na kushindwa kujiajiri wenyewe);
KWA KUWA, kufeli kwa watoto hawa ninaamini siyo kosa lao peke yao bali pia ni kosa la utawala na uongozi wetu, wazazi na jamii kwa ujumla;
NINAAMINI KUWA, kutokuchukua uamuzi wa makusudi na wa lazima kuwasaidia watoto hawa kuwapa nafasi nyingine ni kuwahukumu katika maisha duni na kuwanyima kimsingi nafasi ya kuinuka wakati tayari wameshaanguka
NINAAMINI KUWA, matokeo haya ni dhambi na aibu ya taifa letu hasa katika nchi ambayo inajivunia kuwa ina 'shule nyingi, vyuo vingi, walimu wengi, na teknolojia ya kisasa katika elimu;
NINAAMINI KUWA, Ni jukumu la uongozi wa kisiasa wa taifa kuchukua hatua za haraka na za lazima kuwapa nafasi nyingine watoto hawa kuweza kutengeneza waliposhindwa.
NINAAMINI KUWA, Taifa lina deni kwa watoto hawa, lina deni kwa historia, lina deni kwa familia zao na kwa hakika kabisa lina deni kwa maisha ya watoto hawa. Deni hili tusiliache likue lije kushindwa kulipika. Naamini tunaweza kulilipa kabla halijaanza kuwa na riba isiyokamatika!
Kutokana na mambo yote hayo juu na mengine ambayo nimeyaadhania, ninaamini Utawala wa Rais Kikwete unaitwa na historia, unadaiwa na haki, na unalazimishwa na wajibu kuwapa watoto hawa nafasi nyingine ya kurudia mitihani ya kidato cha nne ili kuweza kuinua alama zao za kufaulu, kusahihisha makosa yao na kuwapa nafasi ya kuweza kuendelea na elimu ya kidato cha tano na cha sita. Kutokana na hili:
HIVYO BASI, Baraza la Mawaziri lifanye kikao cha dharura kuhusiana na matokeo haya ya mitihani ambapo uamuzi wa kutengua matokeo yote ya mtihani uchukuliwe na kuyafuta kabisa matokeo hayo;
NA HIVYO BASI, Baada ya kufuta matokeo hayo serikali iamue kuwa watoto wote waliofanya mtihani huu uliopita watarudia mitihani yote ya kidato cha nne ndani ya mwaka mmoja pamoja na watoto watakaokaa katika mtihani wa mwaka huu au katika mtihani mwingine tofauti
NA HIVYO BASI, Watoto wote ambao katika mtihani huu wamepata daraja la I na II watakuwa na uhuru wa ama kurudia mtihani wao ili kuthibitisha kufaulu kwao au kuendelea na matokeo waliyonayo. Wakiamua kurudia basi kama watafaulu alama za juu zaidi ya sasa watashika alama hizo kama watapata alama za chini watashika alama zao za sasa;
NA HIVYO BASI, Wanafunzi waliopata daraja III na 0 nao itakuwa hivyo hivyo, watapewa nafasi moja ya kurudia mitihani yote kuiinua viwango vyao na wale watakaopata viwango vya juu kuliko vya sasa basi watasika viwango hivyo na wale ambao watapata viwango vya chini kuliko sasa watashika viwango vya sasa.
NA HIVYO BASI, Wanafunzi ambao sasa wamepata daraja la III na 0 endapo watarudia mitihani ijayo na wakainua viwango vyao na kuwa kati ya daraja la I na II basi SERIKALI itawapa nafasi ya kusoma bore kidato cha tano na cha sita katika shule za Sekondari za Serikali. Hii iwe 'AHADI YA TAIFA' (National Promise)
NA HIVYO BASI, ili kutoa motisha kwa shule na walimu ambao wanawafundisha wanafunzi hawa na wengine basi serikali ianze kutoa motisha kwa shule zote (zenye watahiniwa wengi) ambazo zitafaulisha watoto wengi kwenye madaraja ya I na II. Motisha huu utakuwa kwa shule na kwa jopo la walimu wa kidato cha nne.
- Shule ambayo haitatoa daraja 0 kuanzia sasa itapata zawadi ya shilingi milioni 50 kwa matumizi ya sule
- Shule ambayo haitatoa daraja IV kuanzia sasa itapata zawadi ya silingi milioni 75 kwa matumizi yake
- Walimu wanaofundisha shule hizo zikiwa na matokeo hayo watagawana zawadi ya nusu ya tuzo hizo (Milioni 25 kama hakuna 0, milioni 37.5 kama hakuna daraja la IV)
Tuzo hizo zinaweza kurudiwa kila mwaka endapo viwango hivyo vitaendelea.
NA HIVYO BASI, Mwalimu Mkuu wa shule ambazo zinafanya vibaya zaidi watafukuzwa kazi, Afisa Elimu wa Wilaya yenye shule nyingi zilizofanya vibaya nao watafukuzwa kazi.
NA HIVYO BASI, kuanzia sasa wanafunzi wote wanaopata daraja la IV na 0 watakuwa wanapata automatic resit ya mtihani katika mwaka unaofuatia. Na katika hili napendekeza wanafunzi wote waliopata madaraja hayo katika miaka mitano iliyopita na ambao wangependa kurudia mitihani wapewe nafasi hiyo na wao wakifaulu kama hapo juu serikali iwagharimie kidato cha TANO na cha SITA.
PAMOJA NA HAYO, Baraza la Mawaziri liangalie kwa kina haja ya kuufumua mfumo wetu wa elimu kukidhi changamoto ambazo tumeziona sasa. Baadhi ya mabadiliko hayo:
- Kuondoa Elimu kutoka kuwa suala la mfumo wa kitaifa (decentralization of the education system)
- Kuweka miaka mitatu ya kwanza ya elimu kuwa ni ya lazima katika 3R (Hisabati, Kuandika, na Kusoma)
- Kuweka mwaka wa kwanza kwenye O'Level kuwa Wa Kiingereza na Hisabati na Lugha (Pre-Secondary) - miaka mitatu ya mwiso kufanya elimu ya O'level
- Serikali ikutanishe wadau wa elimu kutoka Shule zinazofanya vizuri zaidi kushirikisha mawazo yao na wadau wa shule nyingine (KONGAMANO LA KITAIFA KUHUSU ELIMU - NATIONAL EDUCATION REFORM CONFERENCE)
- Makampuni na taasisi binafsi na za umma zitakiwe kuadopt shule za msingi na za sekondari na yashiriki katika uendeshaji na uboreshaji wake. Mtindo wa sasa wa makampuni makubwa kutoa madawati, mabati halafu wanakimbia haujasaidia kuinua elimu; makampuni yahamasishwe (ikiwemo motisha wa aina fulani katika kodi -tax incentive) kulea shule za sekondari. Tax breaks makampuni yatapata endapo shule wanazozilea hazitakuwa na madaraja ya IV na 0
* Kwa kweli nimeandika kwa haraka bila kufikiria mengi zaidi na implication yake na hivyo ni mchango wangu kidogo tu wa mawazo ya nini tufanye sasa hivi na baadaye. NIna uhakika watu wengine wana mawazo bora zaidi. Jambo moja ambalo hatupaswi kukubali na kuliachilia ni matokeo haya kusimama. Ni LAZIMA yatenguliwe kama tunaamini katika utu, usawa na haki kwa watoto wetu.
KWA KUWA, matokeo ya kidato cha nne ambayo yametoka hivi karibuni yameonesha kufeli kwa kutisha kwa watoto wetu katika mtihani wao;
KWA KUWA, kufeli huko kuna matokeo ya moja kwa moja katika maisha ya wanafunzi hawa, familia zao na kwa taifa kwa u jumla;
KWA KUWA, matokeo hayo ni hasara kubwa kwa wazazi waliowekeza kwa miaka minne ya elimu ya watoto hawa na kwa taifa katika kuwekeza vifaa, walimu na miundo mbalimbali;
KWA KUWA, kuacha kundi kubwa la watoto hawa kurudi katika maisha ya uraiani kutaongeza jamii ya watu ambao hawana elimu ya kutosha na wasioweza kuajiriwa hata katika mifumo isiyo rasmi (pamoja na kushindwa kujiajiri wenyewe);
KWA KUWA, kufeli kwa watoto hawa ninaamini siyo kosa lao peke yao bali pia ni kosa la utawala na uongozi wetu, wazazi na jamii kwa ujumla;
NINAAMINI KUWA, kutokuchukua uamuzi wa makusudi na wa lazima kuwasaidia watoto hawa kuwapa nafasi nyingine ni kuwahukumu katika maisha duni na kuwanyima kimsingi nafasi ya kuinuka wakati tayari wameshaanguka
NINAAMINI KUWA, matokeo haya ni dhambi na aibu ya taifa letu hasa katika nchi ambayo inajivunia kuwa ina 'shule nyingi, vyuo vingi, walimu wengi, na teknolojia ya kisasa katika elimu;
NINAAMINI KUWA, Ni jukumu la uongozi wa kisiasa wa taifa kuchukua hatua za haraka na za lazima kuwapa nafasi nyingine watoto hawa kuweza kutengeneza waliposhindwa.
NINAAMINI KUWA, Taifa lina deni kwa watoto hawa, lina deni kwa historia, lina deni kwa familia zao na kwa hakika kabisa lina deni kwa maisha ya watoto hawa. Deni hili tusiliache likue lije kushindwa kulipika. Naamini tunaweza kulilipa kabla halijaanza kuwa na riba isiyokamatika!
Kutokana na mambo yote hayo juu na mengine ambayo nimeyaadhania, ninaamini Utawala wa Rais Kikwete unaitwa na historia, unadaiwa na haki, na unalazimishwa na wajibu kuwapa watoto hawa nafasi nyingine ya kurudia mitihani ya kidato cha nne ili kuweza kuinua alama zao za kufaulu, kusahihisha makosa yao na kuwapa nafasi ya kuweza kuendelea na elimu ya kidato cha tano na cha sita. Kutokana na hili:
HIVYO BASI, Baraza la Mawaziri lifanye kikao cha dharura kuhusiana na matokeo haya ya mitihani ambapo uamuzi wa kutengua matokeo yote ya mtihani uchukuliwe na kuyafuta kabisa matokeo hayo;
NA HIVYO BASI, Baada ya kufuta matokeo hayo serikali iamue kuwa watoto wote waliofanya mtihani huu uliopita watarudia mitihani yote ya kidato cha nne ndani ya mwaka mmoja pamoja na watoto watakaokaa katika mtihani wa mwaka huu au katika mtihani mwingine tofauti
NA HIVYO BASI, Watoto wote ambao katika mtihani huu wamepata daraja la I na II watakuwa na uhuru wa ama kurudia mtihani wao ili kuthibitisha kufaulu kwao au kuendelea na matokeo waliyonayo. Wakiamua kurudia basi kama watafaulu alama za juu zaidi ya sasa watashika alama hizo kama watapata alama za chini watashika alama zao za sasa;
NA HIVYO BASI, Wanafunzi waliopata daraja III na 0 nao itakuwa hivyo hivyo, watapewa nafasi moja ya kurudia mitihani yote kuiinua viwango vyao na wale watakaopata viwango vya juu kuliko vya sasa basi watasika viwango hivyo na wale ambao watapata viwango vya chini kuliko sasa watashika viwango vya sasa.
NA HIVYO BASI, Wanafunzi ambao sasa wamepata daraja la III na 0 endapo watarudia mitihani ijayo na wakainua viwango vyao na kuwa kati ya daraja la I na II basi SERIKALI itawapa nafasi ya kusoma bore kidato cha tano na cha sita katika shule za Sekondari za Serikali. Hii iwe 'AHADI YA TAIFA' (National Promise)
NA HIVYO BASI, ili kutoa motisha kwa shule na walimu ambao wanawafundisha wanafunzi hawa na wengine basi serikali ianze kutoa motisha kwa shule zote (zenye watahiniwa wengi) ambazo zitafaulisha watoto wengi kwenye madaraja ya I na II. Motisha huu utakuwa kwa shule na kwa jopo la walimu wa kidato cha nne.
- Shule ambayo haitatoa daraja 0 kuanzia sasa itapata zawadi ya shilingi milioni 50 kwa matumizi ya sule
- Shule ambayo haitatoa daraja IV kuanzia sasa itapata zawadi ya silingi milioni 75 kwa matumizi yake
- Walimu wanaofundisha shule hizo zikiwa na matokeo hayo watagawana zawadi ya nusu ya tuzo hizo (Milioni 25 kama hakuna 0, milioni 37.5 kama hakuna daraja la IV)
Tuzo hizo zinaweza kurudiwa kila mwaka endapo viwango hivyo vitaendelea.
NA HIVYO BASI, Mwalimu Mkuu wa shule ambazo zinafanya vibaya zaidi watafukuzwa kazi, Afisa Elimu wa Wilaya yenye shule nyingi zilizofanya vibaya nao watafukuzwa kazi.
NA HIVYO BASI, kuanzia sasa wanafunzi wote wanaopata daraja la IV na 0 watakuwa wanapata automatic resit ya mtihani katika mwaka unaofuatia. Na katika hili napendekeza wanafunzi wote waliopata madaraja hayo katika miaka mitano iliyopita na ambao wangependa kurudia mitihani wapewe nafasi hiyo na wao wakifaulu kama hapo juu serikali iwagharimie kidato cha TANO na cha SITA.
PAMOJA NA HAYO, Baraza la Mawaziri liangalie kwa kina haja ya kuufumua mfumo wetu wa elimu kukidhi changamoto ambazo tumeziona sasa. Baadhi ya mabadiliko hayo:
- Kuondoa Elimu kutoka kuwa suala la mfumo wa kitaifa (decentralization of the education system)
- Kuweka miaka mitatu ya kwanza ya elimu kuwa ni ya lazima katika 3R (Hisabati, Kuandika, na Kusoma)
- Kuweka mwaka wa kwanza kwenye O'Level kuwa Wa Kiingereza na Hisabati na Lugha (Pre-Secondary) - miaka mitatu ya mwiso kufanya elimu ya O'level
- Serikali ikutanishe wadau wa elimu kutoka Shule zinazofanya vizuri zaidi kushirikisha mawazo yao na wadau wa shule nyingine (KONGAMANO LA KITAIFA KUHUSU ELIMU - NATIONAL EDUCATION REFORM CONFERENCE)
- Makampuni na taasisi binafsi na za umma zitakiwe kuadopt shule za msingi na za sekondari na yashiriki katika uendeshaji na uboreshaji wake. Mtindo wa sasa wa makampuni makubwa kutoa madawati, mabati halafu wanakimbia haujasaidia kuinua elimu; makampuni yahamasishwe (ikiwemo motisha wa aina fulani katika kodi -tax incentive) kulea shule za sekondari. Tax breaks makampuni yatapata endapo shule wanazozilea hazitakuwa na madaraja ya IV na 0
* Kwa kweli nimeandika kwa haraka bila kufikiria mengi zaidi na implication yake na hivyo ni mchango wangu kidogo tu wa mawazo ya nini tufanye sasa hivi na baadaye. NIna uhakika watu wengine wana mawazo bora zaidi. Jambo moja ambalo hatupaswi kukubali na kuliachilia ni matokeo haya kusimama. Ni LAZIMA yatenguliwe kama tunaamini katika utu, usawa na haki kwa watoto wetu.
Source :MMM - BGM