Hatimaye Mkurugenzi wa Mashtaka nchini,Eliezer Feleshi amembadilishia shtaka Msanii Elizabeth Michael almaarufu kama Lulu kutoka kuua kwa kukusudia hadi kuua bila ya kukusudia. Lulu anashtakiwa kwa kumuua Msanii mwenzake Marehemu Stephen Kanumba.
Jambo kama hilo lilifanywa pia katika kesi ya Marehemu Kapteni Ukiwaona Ditopile Mzuzuri aliyeshtakiwa kwa kumuua dereva wa daladala kwa kumpiga risasi.
Hii ndio kusema,sasa mlango wa dhamana kwa Lulu uko wazi kwakuwa kosa analoshtakiwa si kati ya yale yasiyo na dhamana. Sinema hii ndio inaelekea patamu, kumbuka kuwa Marehemu Ditopile aliachiwa Huru.
Jambo kama hilo lilifanywa pia katika kesi ya Marehemu Kapteni Ukiwaona Ditopile Mzuzuri aliyeshtakiwa kwa kumuua dereva wa daladala kwa kumpiga risasi.
Hii ndio kusema,sasa mlango wa dhamana kwa Lulu uko wazi kwakuwa kosa analoshtakiwa si kati ya yale yasiyo na dhamana. Sinema hii ndio inaelekea patamu, kumbuka kuwa Marehemu Ditopile aliachiwa Huru.
No comments:
Post a Comment