Pages

Saturday, July 28, 2012

Mahojiano yangu na Zitto kweye Twitter


Kufuatia sakata la baadhi ya wabunge kushutumiwa kwamba wamekula mlungula ili wafanikishe kumuwajibisha waziri wa Nishati na madini na Katibu mkuu wa wizara hiyo, kwa kukiuka sheria za manunuzi ya umma, Nilimtweet Mheshimiwa Zitto Kabwe kuhusiana na kadhia hiyo., Ilikuwa hivi

Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe
Spika ni vema aikubali hoja ya ndg. Vita Kawawa kwamba suala la tuhuma kwa baadhi ya wabunge kuhongwa na lijadiliwe mahususi >>

Mkally Mlanzi@MkallyMlanzi
nakufuatilia sana mheshimiwa,, but kama vile utoe kauli maana these statement they meant u....tunapata shida ss wafuas wako

Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe
usiwe mfuasi wangu. Fuata 'principles' ninazoamini. 'Justice' ndio msingi hapa. Sitatolea kauli tuhuma za kubumbabumba.

Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe
>> kwenye mjadala mahususi ushahidi utatolewa na watuhumiwa kujieleza. Vinginevyo hizi ni siasa tu zenye malengo Maalumu dhidi ya mtu fulani

Mheshimiwa Zitto aliendelea kutweet kwa kumquote Nguli wa mashahiri wa kiswahili Shabani Robert akionesha kushikilia msimamo wa  yale anayoaamini.

Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe
Shabaan Robert alisema, "msema kweli huchukiwa na rafiki zake, sitaona wivu juu ya wale wapendwao na marafiki zao siku zote,">>
Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe
>> 'siwezi kuikana kweli kwa kuchelewa upweke wa kitambo, nikajitenga na furaha ya kweli itakayotokea pale uwongo utakapojitenga.

Jumamosi njema wadau.
Mkali- 0688323837

No comments:

Post a Comment