Pages

Wednesday, July 25, 2012

Makampuni ya simu yaingiza bilioni 43 kwa mwaka kupitia ringtone-Zitto


Mbunge wa Kigoma kaskazini Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe, amesema makampuni ya simu yanajipatia kiasi cha shilingi za Kitanzania Bilioni 43 kupitia Ringtone.

Mh Zitto ameyasema hayo wakati akichangia hotuba ya bajeti ya wizara ya Mawasiliano iliyowasilishwa mapema asubuhi bungeni mjini Dodoma Leo.


Mh Zitto alisema kuwa makampuni ya simu yanapata 80% ya mapato yote yanayolipwa na mteja kwa huduma ya ringtone, 13% kwa makampuni ya kati na 7% ikienda kwa msanii ambaye kimsingi ndiye huangaika na utunzi wa nyimbo.

Mheshimiwa Zitto ameitaja kuwa kampuni ya OWN MOBILE ndiyo inayoendesha biashara hiyo ya ringtone, huku ikiingia mikataba na kampuni ya AIRTEL na VODACOM na kuwa kampuni hiyo mpaka sasa haijasajiliwa.

Mhe amezidi kuishauri serikali kuwa ni lazima wasanii wenyewe wapate si chini ya asilimia 50 ili waweze kufaidika na jasho lao na kulitaka shirika la posta lijiandae kuanza kusambaza kazi za wasanii, ili kupunguza mianya ya rushwa katika kazi za wasanii.

Mkali
0688323837

No comments:

Post a Comment