Mtwara
OFISI ya Mkaguenzi Mkuu wa Afya ya Mimea, imekamata tani 300 za viwatilifu vya ‘salfa’ ya vumbi ambavyo havionyeshi mwaka ulivyotengenezwa wala siku ya mwisho wa kutumika kwake.
Viatilifu hivyo vimekamatwa katika ghala la kampuni moja inayojihusisha na usambazaji wa dawa za kuulia wadudu wanaoshambulia maua ya korosho, lililoko mjini Mtwara.
Kukamatwa kwa kiasi hicho kikubwa cha viwatilifu,kunafuatia ukaguzi wa kushtukiza uliofanywa na Mkaguzi Mkuu wa Afya ya Mimea, Cornelius Mkondo, katika maghala yanayohifadhi viwatilifu hivyo mjini Mtwara.
Viwatilifu hivyo vyenye jina la Falcon-S Dust licha ya kukosa mahali panapoonyesha muda wa kutengenezwa na mwisho wa kutumika, pia vimekutwa vikiwa vikiwa vimeganda mithili ya jiwe ili hali ni kiwatilifu cha vumbi.
Mkondo alisema kumbukumbu zilizopo katika mifuko iliyotumika kuhifadhia dawa hizo, zineonyesha kuwa zimetengenezwa India na zipo kwa majaribio na kwa msingi huo, haziruhusiwi kusambazwa kwa wakulima.
“Hapa zinaonyesha kuwa zipo kwa majaribio, kwa hiyo ni kosa la kisheria kuwasambazia wakulima, zinapaswa kufanyiwa majaribio kwa misimu mitatu halafu mamlaka husika ithibitishe,” alisema.
“Naizuia dawa hii kwa sasa isisambazwe kwa wakulima, nitachukua sampuli kwa ajili ya uchunguzi na kama itabainika kuwa haifai kwa matumzi, itateketezwa na gharama hizo zitakuwa za kampuni hii,” alisisitiza Mkondo.
Hali hiyo imejitokeza wakati madiwani wa Halmshauri ya Wilaya ya Masasi, wakilalamikia kusambaziwa kwa viwafitifu vya vumbi, viliyoganda, jambo linalowalazimisha wakulima kuitwanga kwenye vinu ili wapate unga.
Mmoja wa madiwani hao, Victor Mmavele alisema hivi karibuni katika kikao cha baraza kuwa wakulima wa kata yake ya Nanjota ni miongoni mwa waliokutana na adha hiyo.
Hali ya usambazaji wa pembejeo za ruzuku mkoani Mtwara, inaendelea kuwa tete kiasi cha kusababisha wakulima washindwe kuhudumia mikorosho yao.
Boharia wa kampuni hiyo ya Export Trading, ambayo ni miongoni mwa kampuni zilizopewa zabuni ya kusambaza viwatilifu vya ruzuku vya korosho kwa wakulima, Dismas Mtuhi alikiri kukutwa kwa tani hizo 300 za ‘salfa’ ya vumbi zikiwa zimeganda katika ghala lake na kwamba zilifikishwa katika ghala hilo kwa makosa na kwamba.
Alisema lengo lilikuwa kuzipeleka katika machimbo ya madini.
“Tumezipokea tangu Machi, mwaka huu, baada ya kuziona zimeganda tulizizuia, hatukusambaza kwa wakulima…hizi zililetwa huku kwa makosa, zilikuwa zinaenda machimbo ya madini…zipo tani 300” alisema Mtuhi
OFISI ya Mkaguenzi Mkuu wa Afya ya Mimea, imekamata tani 300 za viwatilifu vya ‘salfa’ ya vumbi ambavyo havionyeshi mwaka ulivyotengenezwa wala siku ya mwisho wa kutumika kwake.
Viatilifu hivyo vimekamatwa katika ghala la kampuni moja inayojihusisha na usambazaji wa dawa za kuulia wadudu wanaoshambulia maua ya korosho, lililoko mjini Mtwara.
Kukamatwa kwa kiasi hicho kikubwa cha viwatilifu,kunafuatia ukaguzi wa kushtukiza uliofanywa na Mkaguzi Mkuu wa Afya ya Mimea, Cornelius Mkondo, katika maghala yanayohifadhi viwatilifu hivyo mjini Mtwara.
Viwatilifu hivyo vyenye jina la Falcon-S Dust licha ya kukosa mahali panapoonyesha muda wa kutengenezwa na mwisho wa kutumika, pia vimekutwa vikiwa vikiwa vimeganda mithili ya jiwe ili hali ni kiwatilifu cha vumbi.
Mkondo alisema kumbukumbu zilizopo katika mifuko iliyotumika kuhifadhia dawa hizo, zineonyesha kuwa zimetengenezwa India na zipo kwa majaribio na kwa msingi huo, haziruhusiwi kusambazwa kwa wakulima.
“Hapa zinaonyesha kuwa zipo kwa majaribio, kwa hiyo ni kosa la kisheria kuwasambazia wakulima, zinapaswa kufanyiwa majaribio kwa misimu mitatu halafu mamlaka husika ithibitishe,” alisema.
“Naizuia dawa hii kwa sasa isisambazwe kwa wakulima, nitachukua sampuli kwa ajili ya uchunguzi na kama itabainika kuwa haifai kwa matumzi, itateketezwa na gharama hizo zitakuwa za kampuni hii,” alisisitiza Mkondo.
Hali hiyo imejitokeza wakati madiwani wa Halmshauri ya Wilaya ya Masasi, wakilalamikia kusambaziwa kwa viwafitifu vya vumbi, viliyoganda, jambo linalowalazimisha wakulima kuitwanga kwenye vinu ili wapate unga.
Mmoja wa madiwani hao, Victor Mmavele alisema hivi karibuni katika kikao cha baraza kuwa wakulima wa kata yake ya Nanjota ni miongoni mwa waliokutana na adha hiyo.
Hali ya usambazaji wa pembejeo za ruzuku mkoani Mtwara, inaendelea kuwa tete kiasi cha kusababisha wakulima washindwe kuhudumia mikorosho yao.
Boharia wa kampuni hiyo ya Export Trading, ambayo ni miongoni mwa kampuni zilizopewa zabuni ya kusambaza viwatilifu vya ruzuku vya korosho kwa wakulima, Dismas Mtuhi alikiri kukutwa kwa tani hizo 300 za ‘salfa’ ya vumbi zikiwa zimeganda katika ghala lake na kwamba zilifikishwa katika ghala hilo kwa makosa na kwamba.
Alisema lengo lilikuwa kuzipeleka katika machimbo ya madini.
“Tumezipokea tangu Machi, mwaka huu, baada ya kuziona zimeganda tulizizuia, hatukusambaza kwa wakulima…hizi zililetwa huku kwa makosa, zilikuwa zinaenda machimbo ya madini…zipo tani 300” alisema Mtuhi
No comments:
Post a Comment