Pages

Friday, July 20, 2012

Zitto aitaka Serikali Kuvirudisha Viwanda vya korosho kwenye Milki yake.



Kaimu mkuu wa kambi ya upinzani bungeni, na mbunge wa Kigoma Kaskazini Mheshimiwa Zitto Kabwe ametaka serikali kuvirudisha haraka viwanda kumi (10) vya korosho vilivyopo mkoani Mtwara katika milki yake.

 Akichangia bajeti ya wizara ya kilimo, iliyowasilishwa mapema asubuhi hii ya leo, Zitto amesema wamiliki wa viwanda hivyo wameshindwa kuviendesha viwanda hivyo kulingana na sheria za ubinafshaji.

Mheshimiwa Zitto amesema Tanzania huuza korosho ghafi kwa zaidi ya asilimia themanini (80%) nchi za nje bila ya kuziongezea thamani. Kwa kufanya hivyo Watanzania wengi wanakosa ajira ambazo wangezipata kupitia viwanda ambavyo vingeongeza thamani ya zao hilo.

Mkali
0688323837

No comments:

Post a Comment