CENTENNIAL, Colo. (AP) --
Mwendesha mashtaka wa colorado amemsomea mashtaka ya mauaji 24 na mengine ya kujaribu kuua 116, mhitimu wa wa fani ya neuroscince, leo siku ya jumatatu katika mashambulizi ya kustukiza yaliofanyika katika maonesho ya filamu mpya iitwayo Batman huko colorado.
James Holmes ambaye alionekana kama amechanganyikiwa kwa mara ya kwanza alipojitokeza mahakamani wiki iliyopita,aliweza kubadilishana mawazo na mmoja wa mawakili wake mahakamani hapo. Mwenendo wa kesi hiyo mpaka sasa bado haujulikani vizuri.
Mashambulizi hayo ya usiku yaliacha watu 12 wakipoteza maisha na 58 wakijeruhiwa vibaya. Baada ya kukamatwa kwake polisi walisema makazi ya kijana huyo si ya kawaida, na moja ya mashtaka alosomewa leo hii ni kukutwa na vitu vya mlipuko. Wachunguzi wa mambo ya kisheria wamesema kesi hiyo itagubikwa na ushindani wa hoja ya kuhusiana na akili ya kijana huyo kama ni punguani ama la.
Source: Reuters
Translation: Mkali
No comments:
Post a Comment