Pages

Wednesday, July 18, 2012

Watu saba wafariki dunia kwenye ajali ya meli Zanzibar


Waziri Emmanuel Nchimbi akiongea na TBC1 amesema “vikosi vya uokoaji vinaongozwa na mkuu wa jeshi la polisi Inspekta Jenerali Said Mwema vinaendelea na uokoaji”
Kuhusu watu waliopoteza maisha au kuokolewa Waziri Nchimbi amesema “Katika abiria wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 250 waliokua wamebebwa na boti hiyo, wameokolewa 124 wakiwa hai na waliothibitishwa na jeshi la polisi kufariki dunia ni saba tu, juhudi kubwa za uokoaji zinaendelea”

Chanzo: TBC 1.

No comments:

Post a Comment