Pages

Saturday, July 21, 2012

Naibu spika Ndugai apindisha kanuni tena


Naibu spika wa bunge la jamhuri ya muungano Mh Job Ndugai leo amepindisha kanuni waziwazi kufuatia hoja iliyotolewa na Mbunge wa kuteuliwa, ndugu James Mbatia kuhusu kuahirisha bunge.

Mheshimiwa Mbatia alitoa hoja hiyo mara tu waziri wa kilimo chakula na ushirika Mh chizza kumaliza kutoa majumuisho ya bajeti ya wizara yake.

Mh Mbatia alisema kwa kuwa idadi ya wabunge waliopo bungeni haifiki nusu ya wabunge ambao ni 176 kwa muda huo, kanuni haielekezi bunge kuendelea kufanya maamuzi ya kupitisha bajeti ya wizara hiyo.

Hoja hiyo iliungwa mkono na Mbunge Mkosamali pamoja na Machali lakini Naibu spika aliamuru bunge kuendelea na kikao hicho. Kuona hivyo mnadhimu mkuu wa upinzani Ndugu Tundu lissu nae alisimama kuendelea kuomba kanuni hiyo kufuatwa lakini dhahiri shahiri Naibu spika alionekana wazi kutopendelea suala hilo kufanyika.

Chanzo- TBC LIVE - Bungeni leo
Mkali

No comments:

Post a Comment